Search for Podcasts
Trumix.com
Our New Site
Internet Radio
Podcasts
Create a Playlist


Podcast Directory:
Browse Podcasts
Add your Podcast
Remove a Podcast
Search for Podcasts
Podcast Directory
by Country
by Language
by Buzz
by Popularity
by Category
by Tags
by Region
by City
on a Google Map



Podcast Help:
What is Podcasting
Creating an XML
Podcast Hosting
Podcast Software
Firefox Plugin
Podcast Hardware




About Us:
Podcast Advertising
Contact Us
Copyright Issues
Help Wanted




Internet Radio:
Find
State
Country
Language
Music
Sports
Regions
Popularity

Discount Gold Offer

Stiletto New Price

Free Graphics


Sauti ya Mwanakijiji Podcasts

PodcastDirectory / News and Politics / News
PodcastDirectory / Regions / AF / Tanzania

Primary Format :
News

Also Listed as:
News

City :
Mwanza
State/Province :
Unknown
Country :
Tanzania
Country :
AF
User Tags:

User Votes:

RSS Feed
Website

People found this Podcast
Searching for:

Tanzania News | news |

View this Podcast on a Google Map.

Add to iTunes

Text Only listing of Sauti ya Mwanakijiji Podcasts

Trumix.com listings available of Sauti ya Mwanakijiji Podcasts

Click Here to Update the directory of this podcasts programs.

Trumix.com listings available of Sauti ya Mwanakijiji Podcasts
Build your own playlists with this podcast.


Rostam na Mtikila na kisa cha Milioni 3!

Mbunge wa Igunga Mhe. Rostam Aziz mapema leo amezungumza na waandishi wa habari akijibu kitendo cha Kanisa la KKKT kumkana na kutaka kumrudishia mchango alioutoa kusaidia Kwaya ya "Amkeni" ya Usharika wa Kinondoni. Katika majibu yake Bw. Rostam (CCM) ametoa madai makubwa pia likiwemo la kudai kuwa yeye amekuwa akisaidia makanisa na misikiti likiwemo Kanisa la Mchg. Christopher Mtikila. Bw. Rostam amedai kuwa miezi mitatu iliyopita Mchg. Mtikila alienda kwake ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Uhuru wa Taasisi zetu, kiini cha Utawala wa sheria!

UCHUNGUZI WA BUNGE MFANO MBAYA WA UCHUNGUZI HURU Jeshi la Polisi limetoa ripoti yake kuhusu uchunguzi wa kile kilichodaiwa vitendo vya kishirikina Bungeni karibu mwezi mmoja uliopita ambapo ilidaiwa mmojawapo wa wabunge alionekana akimwaga unga kwenye viti mbalimbali. Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma amesema kuwa (kati ya niliyoyanasa kwa haraka) a. Hakuna Kamera iliyozimwa kuanzia mwaka 2006 (don't ask me walisema zilikuwa zimezimwa) b. Kwenye mkanda uliodaiwa hakuna mtu aliyeonekana ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Cheyo: "Serikali isilisingizie JWTZ kuhusu Meremeta"

Mwishoni mwa juma nilipata nafasi ya kuzungumza na Mbunge wa Bariadi Mashariki Mhe. John Momose Cheyo (UDP) kuhusu suala la kampuni ya Meremeta ambayo imepokea mabilioni ya shilingi toka Benki Kuu na hakuna mtu aliye tayari kusema wazi kampuni hiyo ni ya nani. Mahojiano yangu na Bw. Cheyo yalikuja masaa machacha baada ya majibizano yake na Waziri Mkuu Mhe. Pinda Bungeni siku ya Ijumaa ambapo alikataa kuyakubali maelezo ya Waziri Mkuu kuwa kampuni ya Meremeta na nyingine yenye kuhusiana naz ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Chenge ahusishwa na Ushirikina!

Tafadhali soma habari kamili kwenye http://www.klhnews.com Wakati huo huo tumeanza kutangaza "live" kama majaribio kwa kucheza muziki. Tunaomba feedback yako mahali popote unapotusikia na kama unatusikia vizuri, na hasa wale walioko Tanzania.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Leo ni Siku ya Bajeti - Jisomee kabla ya kusikia!

Leo ni siku ya Bajeti. Waziri wa Fedha Bw. Mustafa Mkullo anatarajiwa kusoma bajeti hiyo leo na hivyo kuonesha ni wapi tumefika toka mwaka uliopita na wapi tunataka kwenda katika mwaka ujao wa fedha. Nimepata nafasi ya kupata nakala ya bajeti hiyo ambayo inapatikana hapa: http://www.jamiiforums.com/attachment.php?attachmentid=1680&d=1213211256 Tafadhali copy and paste kwenye browser yako. Nimatumaini yangu mtapata nafasi ya kuipitia kabla hamjaisikia.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Huu si wakati wa kukata tamaa!

Bila ya shaka mlolongo wa matukio kadha wa kadha unaweza kumfanya mtu yeyote kushika tama na kukata tamaa. Hasa inapotokea matukio ambayo yanaihusu nchi yetu. Msururu wa kashfa ambazo zimeiandama nchi na viongozi wetu bila ya shaka vinaweza kukufanya ujisikie mpweke na mnyonge na zaidi kuweza kujiuliza "Tanzania ina matatizo gani?". Kwa wengine kujiuliza swali hili kunaendana na hisia ya kuachwa peke (abandonment) na kukata tamaa (despair). Na zaidi ya yote kuna wengine ambao wanaweza kuj ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Exclusive: Mhe. Anne Kilango Malecela azungumza na KLHN

Tulikokuwa tunaenda siko, tumeamua kugeuka" - hayo ni baadhi ya maneno ya Mhe. Anne Kilango Malecela akizungumza na KLH News siku chache zilizopita akielezea mabadiliko ya wabunge wa CCM linapokuja suala la kulinda maslahi ya Taifa. Kati ya mambo ambayo anayazungumzia ni pamoja na hali ya kisiasa nchini, kifo cha Ballali, kwanini wabunge wa CCM walikuwa wanaitetea serikali yao hata ilipokuwa inaharibu, kwanini anaamini Kikwete ni kweli anataka mabadiliko na ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Wabunge wahoji kifo cha Ballali

Hii ni marudio ya show tuliyofanya siku ya Jumapili. NI sehemu tu ya onesho hilo.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Gov. Balali Afariki Dunia

Aliyewahi kuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania Dr. Daud Balali amefariki dunia. Habari ambazo zimeanza kusikika tangu jana jioni na kuthibitishwa na ndugu zake zimesema kuwa Gavana Balali amefariki mwishoni mwa juma na mipango ya mazishi inafanywa. Anatarajiwa kuzikwa huko huko Marekani. Inatarajiwa taarifa ya kifo chake kutangazwa Tanzania baadaye leo. Sikiliza matangazo kuhusu kifo hicho hapa au kwa kutwa nzima ya kesho tutakuwa tunaleta maendeleo yoyote ya habari hii kwenye tovuti yetu y ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Alichozungumza Mhe Zitto Detroit!

Karibu wiki moja iliyopita Mhe. Zitto Kabwe alizungumza na jumuiya ya Watanzania waishio Jimbo la Michigan nchini Marekani. Mazungumzo hayo yaliyofanyika wakati wa hafla ya chakula cha jioni aliyoandaliwa Bw. Zitto yaligusia mambo mbalimbali na hasa kuwataarifu wanajumuiya hiyo mambo mbalimbali yanayoendelea nyumbani na pia kusikiliza maoni na maswali yao. Matangazo ya leo basi ni hotuba ya Mhe. Zitto kwa jumuiya hiyo na sehemu ya maswali na majibu, yote ni uncut and an edited. Makosa meng ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Nimevunja Mwiko - Soma "Kulikoni" la Leo

Kwa karibu wiki mbili sasa nimekuwa nikitengeneza hoja na kumulika kama vile kurunzi idara ya Usalama wa Taifa. Sikiliza introduction ya makala yangu maalum kwenye gazeti la "Kulikoni" leo. Kwa wale ambao hampo nyumbani makala hii itawekwa baadaye mchana wa Ijumaa (saa za Marekani) kwenye http://www.klhnews.com upande wa editorial.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Chenge - mbona anatuchengua!?

Chenge ni bilionea wa kutupwa ambaye kwake shilingi Bilioni moja anayodaiwa kuificha huko Marekani ni sawa na "vijisenti" vichache. Hivi tatizo letu liko wapi? Je yawezekena kuwa chenge ni dalili tu ya tatizo? Je eye ni kiongozi pekee wa TAnzania ambaye amewekeza mabilioni ya shilingi kwenye akaunti za kigeni? Je ajiuzulu au na yeye anaweza akalia kuwa amefanywa "Bangusilo" wa rada!?

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


KLH Exclusive: "Mafuriko Kyela - 40,000 hatarini!" - Dr. Harrison Mwakyembe

Pichani baadhi ya wananchi wakijaribu kuvuka mto. Kidaraja hicho sasa hakipitiki tena. Picha kwa hisani ya Mjengwa Mvua za masika zimezidi kupamba moto nchini na zimekuwa zikisababisha mafuriko sehemu mbalimbali. Baadhi ya maeneo ambayo yamepata mafuriko ni pamoja na Vunjo, Same na Kyela. Hata hivyo hadi hivi sasa ni wilaya ya Kyela ambayo ina kata 15 ambazo kati ya hizo 11 zimepatwa na mafuriko makubwa . Siku ya Jumamosi nimepata nafasi ya kuzungumza na Mbunge wa Jimbo la Kyela Dr. Harr ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Bila CCM Madhubuti? - Mwalimu alisema kweli...

Mwanzoni sikuyaelewa maneno ya Baba wa Taifa Mwl. J.K. Nyerere kuwa “Bila CCM Madhubuti nchi yetu itayumba”. Nilifirikia kuwa alimaanisha “Bila CCM” nchi yetu itayumba, na pia nilidhania alimaanisha kuwa “Bila viongozi wa CCM” nchi yetu itayumba. Miaka hii ilivyopita na hasa baada ya matukio yaliyolikumba Taifa letu ndio maana hasa ya maneno yake imeanza kuniingia na kwa hakika nimekubali kuwa bila Chama cha Mapinduzi ambacho ni “madhubuti” basi Taifa letu liko matatani, na ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Operesheni Demokrasia Comoro - Wangwe angekaa kimya!

Saa na wakati huu vikosi vya majeshi ya Jumuiya ya Afrika vimeanza mapambano ya kukikomboa kisiwa cha Anjouan ili hatimaye kurudi katika shirikisho la Comoro. Vikosi hivyo vikiongozwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania wanashiriki katika Operesheni Demokrasia Komoro yenye lengo la kumuondoa Rais aliyejipachika Bw. Mohammed Bacar. Hivyo saa na wakati kama huu ambapo vijana wetu wako katika hali ya hatari na ambapo wanayaweka maisha yao hatarini ni kitendo cha kutokuwajibika kwa mwanasiasa kam ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Sisi tumepotea wapi?

Ndugu zangu, mlolongo wa matukio ambayo yameliandama Taifa letu kwa miaka kadhaa sasa na ambayo kilele chake bado hatujui kitafikia lini yanathibitisha jambo moja kubwa, kwamba sisi kama Taifa kuna mahali tumekwenda kombo. Kuna mahali ambapo sisi kama taifa tumepotea njia na hatuko tayari kukubali kuwa tumepotea na matokeo yake tumeendelea kufuata njia ile ile ya upotevu tukiamini kuwa huko mbeleni mambo yatanyoka. Je, Tanzania tunayoiona leo hii, ndiyo hii ambayo tuliitaka na ambayo waze ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Walioiba EPA wasiepe Pingu!

Habari za kuwa wale walioifanya uhalifu kwenye akaunti ya EPA wameanza kurudisha fedha zile zimepokelewa kwa hisia zinazopingana. Kuna wale ambao wanaona uamuzi huo ni wa kupongeza kuwa "angalau fedha zinarudi" na hawa wanasema kuwa baada ya fedha kurudi ndiyo tufuatilie suala la kupelekwa wahalifu hawa mahakamani. Kuna wale wengine ambao wanaamini kuwa fedha kurudishwa kungeenda sambamba na wahalifu kuchukuliwa hatua za kisheria badala ya ilivyo sasa. Watu hawa nikiwemo mimi naamini tun ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Mahojiano na DCI : "Jambo Forums haihusiani na Ughaidi"

Baada ya msemaji wa Jeshi la Polisi kuihusisha Jambo Forums na Ughaidi niliamua kutafuta msimamo wa wale wanaochunguza ili watuambie kweli wana amini kuwa JF inahusiana na Ughaidi. Nilipata nafasi ya kuzungumza na Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DCI) Kamanda Robert Manumba na kumuuliza mambo kadhaa yanayohusiana na Jambo Forums na kukamatwa kwa wawili kati ya wanachama wake kama 4000. Tafadhali karibu usikilize mahojiano hayo na kwa habarii za kutwa nzima usikose kuingia http://www.klhnew ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Jambo Forums na Ughaidi?

Jana ilikuwa ni siku ya huzuni katika jitihada za kupanua uhuru wa habari na maoni Tanzania; jeshi la Polisi lilikiri kuwa linawashikilia watu wawili kutokana na kuhusika kwao na JF kwa madai kuwa tovuti hiyo inahusiana na uchochezi na mambo ya Kighaidi. Inasikitisha kuona kuwa Jeshi letu la Polisi badala ya kuwakamata watu waliokwapua fedha za umma na ambao wameliingizia Taifa letu hasara limeamua kuwatafuta watu walioufunua ufisadi hadharani. Hili limesikitisha sana. Ni kwa sababu hiyo w ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Mizengo Pinda Waziri Mkuu mteule

Pichani Waziri Mkuu Mteule Bw. Mizengo Pinda akipongezwa na wabunge mara baada ya kulipitisha jina lake kuwa Waziri Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Mhe. Mizengo Pinda (Mpanda Mashariki) kuwa Waziri Mkuu mpya kuchukua nafasi ya Mhe. Edward Lowassa aliyejiuzulu kufuatia kashfa ya Richmond. KLH News international inakuletea taarifa ya uteuzi huo hapa kwenye podomatic na pia kwenye http://www.klhnews.com ambapo tunafuatilia maendeleo ya sakata hili linalojifunua kila baada ya masaa ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Lowassa aandika barua ya kujiuzulu- JK atakubali?

Tafadhali sikiliza maoni yangu kuhusu hili. Na zaidi ya yote hakikisha unatembelea KLH News through out the day for any breaking news and for any new development kufuatia kashfa hii ya Richmond. Ukienda kwenye "Archives" hapa utaweza kusikiliza mahojiano yangu na Dr. Mwakyembe miezi michache iliyopita. Pichani Mbunge wa Kyela - CCM na Mwenyekiti wa Kamati iliyochunguza Richmond Mhe. Dr. Harrison Mwakyembe akitopewa mkono wa pongezi (pole?) na wabunge wenzake. Picha kwa hisani ya Mroki Mro ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Wabunge wanaokurupuka, na Kampeni za Kiteto

Leo hii vichwa vya habari vya magazeti mengi nyumbani vinahusu jinsi wabunge walivyodai ripoti kamili ya uchunguzi wa BoT badala ya maelezo ya juu yaliyotolewa na Waziri wa Fedha Bi. Zakia Meghji Bungeni jana. Binafsi siyo tu nasikia kinyaa lakini nakerwa na wabunge ambao kama watu walioamshwa usingizini wanakurupuka na kuanza kujifanya ati leo wamekuwa watetezi wa BoT Wabunge hawa walikuwa wapi wakati wa miaka 15 ya ufisadi kwenye benki yetu Kuu? Walikuwa wapi wakati Meremeta na ndugu za ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Tumepigwa ganzi ya Ufisadi?

Mlolongo wa kashfa umeigubika serikali ya Tanzania na kama vile watu wanashindana imekuwa ni kashfa juu ya kashfa. Swali ambalo linanisumbua hasa baada ya kashfa ya BoT naona watu wamekuwa kama wametiwa ganzi ya aina fulani, kuwa hatusikii tena uchungu na tumekubali kuwa "mambo ndivyo yalivyo" Je tukubali kuwa tuko katika utamaduni wa kifisadi na mambo ndivyo yalivyo? Je tukubali kuwa sisi sote ni mafisadi wa aina moja au nyingine na tukipewa nafasi hizo walizonazo wao bila ya shaka na ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Mahojiano na Waziri wa Fedha Bi. Zakia Meghji (MB)

Je, Bi. Zakia Meghji naye ni fisadi? Je kitendo chake cha kuandika barua kuthibitisha malipo kwa kampuni iliyotajwa kwenye ripoti ya BoT na baadaye kuikana barua hiyo baada ya kufahamu ukweli ni kitendo cha kifisadi? Je, anapaswa kujiuzulu? Nimezungumza na waziri wetu wa fedha kujaribu kutafuta baadhi ya majibu ya maswali hayo. Sikiliiza na uamue mwenyewe. Kama huwezi kusikiliza hapa kwa sababu yeyote ile, unaweza kusikiliza mahojiano haya kwenye http://www.klhnews.com eneo la podcast pal ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Ripoti ya Kamati Teule kuhusu Richmond, wananchi wasubiri!

Hatimaye Ripoti ya uchunguzi kuhusu kampuni ya Richmond Development ya Houston imekamilika na hatimaye kukabidhiwa rasmi kwa Spika wa Jamhuri ya Muungano hapo jana na Mwenyekiti wa Kamati Teule ya Bunge Dr. Harrison Mwakyembe (Kyela - CCM) pichani. Kamati hiyo imetumia siku 45, mashahidi 75, vielelezo zaidi ya mia moja na maswali zaidi ya 2700. Kwa kifupi ni kuwa ukilinganisha na uchunguzi wa PCCB inawezekana wananchi watataka Kamati Teule ifanye uchunguzi wa mambo mengine yote kuliko Taas ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Heri ya Krismasi !

Wapendwa wasikilizaji kwa niaba yangu na ya KLH News napenda kuwatakia ndugu zetu Wakristu mahali pote duniani na wengine wote heri ya Krismasi wanapoadhimisha kuzaliwa kwa Mkombozi Bwana Yesu Kristu. Kutoka hapa kijijini na kwenu nyote nawatakia heri ya Krismasi. Mnayoisikiliza ni kwaya ya Vijana ya Kanisa Katoliki la Mtakatifu Theresa Arusha mjini. Albamu yao inatoka hivi karibuni na bila ya shaka kwa watakaopenda wanaweza kuwasiliana nami kuona jinsi gani wataweza kuinunua.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Eid Mubarak!

Napenda kutumia nafasi hii kuwatakia heri ya siku kuu ya Eid ndugu zetu waislamu wanapoungana na na Waislamu wengine katika kuunganisha mioyo yao katika kuhitimisha mojawapo ya Nguzo za Uislamu, yaani Hijja. Tunapowafikiria wale waliokuwa wamekwama uwanja wa ndege tuna matumaini kuwa serikali imefanya mipango mizuri na ya uhakika ili kuweza kuwarudisha wote salama na bila ya usumbufu wowote ule.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Mahojiano na Jaji Mark Bomani wa Kamati ya Madini

Yafuatayo ni mahojiano yangu na Jaji Mark Bomani, Mwenyekiti wa Kamati ya Ushauri ya Rais kuhusu Sekta ya Madini. Nilipata nafasi ya kuzungumza naye kuhusu kamati hiyo na majukumu yake. Majibu ya Jaji Makani yanaweza kuwashangaza watu wengi. Zaidi ya yote miaka 46 baada ya Uhuru; wapi tulipo, wapi tunataka kwenda. (Pichani, Amir Jamal, Dereck Brycson, JK Nyerere, Chief Abdallah Fundikira, Gorge Kahama Nyuma: Kushoto Solomon Eliofoo, Rashid Kawawa, Nsilo Swai, Oscar Kambona, Tewa Saidi Tew ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Mkapa na Yona wanyang'anywe Kiwira?

Wakiwa madarakani Rais Benjamini Mkapa na Waziri wake wa Nishati na Madini waliingia ubia na kuanzisha kampuni ya Tanpower Resources. Wakati Yona analiambia Bunge kuwa wanatafuta wawekezaji wa "kufufua" Mgodi wa Makaa ya Mawe wa Kiwira, sirini walikuwa wanapanga yeye na Rais wake kuwa "wawekezaji" hao watakuwa ni wao wawili. Na miezi michache kabla Rais Mkapa hajaachia madaraka, Mgodi wa Kiwira ulikuwa chini ya viongozi hao wawili wakiwa na hisa zaidi ya asilimia 80. Hadi leo hii hakuna ali ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Buriani mzee Kanyama Chiume...

Most of us knew his name by reading his articles and opinions in Mzalendo, Daily News and Uhuru; He was one of the leading nationalists of his time and indeed a patriot of Africa, a true son of our beloved motherland. Mr. Chiume who was born in Malawi and later exiled to Tanzania was a "leader of Nyasaland African Congress and served as the Minister of Education and the Minister for Foreign Affairs in the 1960s." according to one popular website. Beside writing for Tanzania Newspaper he als ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Salamu kwa Siku ya Wanafunzi Duniani - Ukumbi wa DDC

Leo kama mnavyofahamu kulikuwa na makongamano ya wanafunzi jijini Dar-es-Salaam. Moja lilifanyika Ukumbi wa Ubungo Plaza na kuhutubiwa na Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Mhe. Pius Msekwa na lile jingine lililofanyika Ukumbi wa DDC na kuhutubiwa na wasomi mbalimbali na viongozi wa chama cha Demokrasia na Maendeleo akiwemo Mhe. Zitto Kabwe. Nilipata nafasi ya kutuma salamu za mshikamano kwa kongamano la DDC baada ya kuombwa kutuma ujumbe huko. Walioko nyumbani waliupata kwa njia ya maandishi, ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Tuwakatalie watawala wetu?

Wakati umeanza kufika ambapo wananchi waanze kuwakatalia watawala wao!! Nisikilize leo nikifafanua kwanini tuanze kuwakatalia na ni vitu gani hivyo vya kukataa!

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Hongera Mheshimiwa Spika.....

WATANZANIA hatuna budi kupiga vigelegele, makofi na hoihoi za shangwe! Hatuna budi kucheza mdundiko, lizombe, gita, mganda, na mdumange! Hatuna budi kutunga tenzi, ngonjera na nyimbo za sifa kwani Spika wetu, amevaa vazi lenye michirizi ya dhahabu lililochirizwa Ulaya! Kuna wakati hatuna budi kuondoa tofauti zetu za kisiasa, na hasa wivu usio na msingi, hasa tunapoona mwenzetu amefanikiwa. Si tu kuziondoa na kuziweka pembeni tofauti hizo, bali hata kuzizika na kuzisahau kabisa hasa inapoto ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


~ * ~ The Spoken Word - "I Can't Wait" ~ * ~

By. M. M. mwanakijiji Wondering, and hoping, and praying That it’ll all be alright! That my country will rise and be A nation, and it will take its place among the nations Of the World and it’ll be a rightful place. But our rulers keep telling us, just wait! ]They tell us to wait, When we ask about corruption, And when we question their intentions They come back with political intimidation That if we don’t stop, there’ll be a confrontation, So they tell us people! just wait! ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


KLH Exclusive: Mahojiano na Dr. Salim Ahmed Salim

Tarehe 14 Oktoba 2007 ni miaka nane kamili, tangu Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere atutoke na kutuacha wakiwa. Kati ya viongozi na watanzania wachache waliopata kumfahamu Mwalimu kwa karibu na kuwa wasaidizi wake wa karibu ni Dr. Salim A. Salim ambaye aliwahi kushika nafasi mbalimbali za uongozi katika serikali ya Zanzibar na baadaye katika serikali ya Muungano. Baadhi ya nafasi ambazo aliwahi kushika ni pamoja na Ubalozi, Uwaziri (akiwa Waziri Mkuu, Waziri wa Mambo ya Nchi ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Eid Mubarak kwenu Nyote!!!

Napenda kutumia nafasi hii kuwatakia ndugu zetu Waislamu wa Tanzania wanapoungana na Waislamu wengine pote duniani kuadhimisha siku kuu hii ya Eid el Fitr wanapomalizia mfungo Mtukufu wa Ramadhani. Siku ya Jumapili tunatarajia kuwa na matangazo "live" kupitia Bongoradio.com tunapoadhimisha miaka nane tangu Baba wa Taifa atutoke. Hivyo usikose matangazo hayo kuanzia kama saa nane mchana EST sawa na saa tatu za Usiku EAT. Kwa wale Wakristu na watu wa imani nyingine nawakaribisha kwenye ukura ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Nyerere: " Ikulu ni Mzigo, kwanini wanakukimbilia?"

Hii ni sehemu ya pili ya Hotuba ya Mwalimu Mei Mosi 1995. Hapa ndipo alipokuwa mwiba wa serikali ya CCM hasa baada ya kudai kuwa wameacha "Mambo ya Msingi" . Ni katika sehemu hii lile swali muhimu la "kuna biashara gani Ikulu" liliulizwa. NImefanya editing zaidi kidogo ya kupunguza sauti za watu uwanjani ili mwalimu asikike vizuri na ningekuwa na muda zaidi kidogo ningefanya bora zaidi, mniwie radhi kwa mwangwi kidogo.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Nyerere Mei Mosi '95: "Watanzania Mjomba wenu ni nani?"

Ifuatayo ni sehemu ya kwanza ya hotuba aliyoitoa Baba wa Taifa kwenye sherehe za Mei Mosi 1995. Tunapokumbuka miaka nane tangu Mwalimu Nyerere afariki hatuna budi kupitia japo kwa hatua hazina ya hekima yake. Wakati anatoa hotuba hii mwaka 1994 kulikuwa na mgomo wa wafanyakazi, na mwaka 1995 ulikuwa ni mwaka wa uchaguzi na huo ukiwa ni uchaguzi wa kwanza baada ya kurejesha tena mfumo wa vyama vingi. Hivyo, Mwalimu alipokuwa anatoa hotuba hii watu wengi walikuwa wanaonesha nia ya kutaka kw ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Mhe. Moh'd Seif Khatib: "Viongozi hawazomewi, ni uongo!"

Siku ya Jumamosi kwenye matangazo yetu ya moja kwa moja (live) nilipata nafasi ya kuzungumza na Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo wa Serikali ya Tanzania Mhe. Mohammed Seif Khatib (MB). Makubwa tuliyozungumza ni suala zima la tuhuma zilizotolewa na ushirika wa wapinzani tarehe 15 Septemba pale Jijini Dar. Pamoja na hayo tulizungumzia kuhusu suala la Buzwagi na jinsi mwitikio wa wananchi ulivyokuwa na hasa ziara ambazo zimefanywa wiki iliyopita na Mawaziri na Manaibu wao kwenye mikoa ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


"Majibu ya serikali hayatoshelezi" - Mahojiano na Tundu Lissu

Siku ya Jumamosi nilipata nafasi ya kuzungumza kwa kirefu na mwanaharakati wa mazingira na mwanasheria wa Chadema ambaye pia ni Wakili katika Mahakama Kuu ya Tanzania Bw. Tundu Lissu. Katika mazungumzo yetu ambayo yalirushwa moja kwa moja (live) kupitia Bongoradio.com tulizungumzia madai ya wapinzani na mkataba wa Buzwagi ambao Bw. Lissu ndiye aliuchambua hadharani kwenye kipindi cha "Jenerali on Mondays". Mahojiano haya ni karibu saa nzima.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


CCM ikubali tatizo kwanza...!!

Tangia sakala la "orodha ya ufisadi" lianze, serikali ya CCM imekuwa ikitoa majibu ya kukanganyana na mengine hayaingii akili hata kidogo. Majibu mengine yamejaa kiburi na dharau na mengine inabidi mtu ajiulize "walikuwa wanafikiria nini". Kwa maoni yangu kabla ya viongozi wa serikali na wa CCM kuanza kutoa majibu kuhusu tuhuma kwa viongozi 11, la kwanza ambalo wangelifanya ni kukubali tatizo kwanza, hiki kiburi wanachokionesha kuwa wao hawawezi kukosea na wengine wanadai kuwa wamekuwa w ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Nini kimemsibu Jaji Warioba?

Kama ripoti iliyoandikwa na gazeti la Habari Leo ina ukweli basi kuna kitu kinachoendelea na ambacho bila ya shaka kimemsibu Jaji Warioba kuja na mawazo ya aina hii. Hebu soma na uamue mwenyewe au ni mimi ndiyo nimechanganyikiwa. [b]Mgaya Kingoba HabariLeo; Friday,September 28, 2007 @00:02[/b] WAZIRI Mkuu mstaafu, Jaji Joseph Warioba amesema amekerwa na tabia ya wanasiasa kupakana matope na kuonya kuwa kisingizio cha utawala bora kisitumiwe kutaka kuangusha dola zilizopo madarakani. “T ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Tundu Lissu auchambua Mkataba wa Buzwagi

NInawaletea mahojiano ya Mwanasheria maarufu nchini anayeshughulika na Haki za Binadamu na Masuala ya Mazingira na pia anayefuatilia masuala ya madini Bw. Tundu LIssu. Mahojiano hayo yalirushwa moja kwa moja na Channel Ten na kwa msaada wa mtazamaji CMB wa Jambo Forums tunaweza kuyaletea hapa mahojiano hayo. Sikiliza kwa makini na uamue. Pia tunajitahidi kupata nakala ya mkataba huo. Kwa wale walioko nyumbani mnaweza kusoma juu ya Mkataba huo kwenye magazeti ya "This Day" na "Kulikoni" na b ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


CCM isipuuzie hoja za Wapinzani, wazijibu!

Uongozi wa Chama cha Mapinduzi umeamua kuwa hoja zilizotolewa na watanzania kuhusu masuala mbalimbali hazistahili kujibiwa. Kwa mujibu wa Katibu wa Idara ya Uenezi na Itikadi ya Chama hicho Mhe. Aggrey Mwanri MB (CCM - Siha) CCM haitaenda mahakamani bali itaenda kwa wananchi na kujibu hoja za watanzania hao kwa kuwataka wananchi wazipuuze hoja hizo. Miongoni mwa hoja ambazo Mhe. Mwanri anataka wananchi wazipuuzie ni zile zile za Ubadhirifu wa Benki Kuu, Mikataba ya Madini hususan ule wa Buz ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Rais Mkapa na Matumizi mabaya ya Ikulu - Dr. Slaa

Ifuatayo ni sehemu ya pili ya mahojiano yangu Dr. Slaa kufuatia mkutano wao mkubwa uliofanyika mwishoni mwa wiki. Nimeambatanisha pia orodha na maelezo mliyoyasikia kwenye mahojiano haya ili uweze kupitia moja baada ya nyingine na uweze kutolea maamuzi wewe mwenyewe. Bonyeza Hapa Kudownload

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Kukamatwa wabunge wa CCM, Ishara ya Nyakati?

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa imewatia mbaroni viongozi kadhaa wa Chama cha Mapinduzi kwa tuhuma za kujihusisha na vitendo vya rushwa. Miongoni mwao ni wabunge Michael Laizer wa Longido na Elisa Mollel wa Arumeru Mashariki. Hii ni mara ya kwanza katika miaka ya hivi karibuni kuwa Chama cha Mapinduzi kiko tayari kuwatosha baadhi ya viongozi wake wakubwa. Je inawezekana huu ni mwanzo wa nyakati mpya na ni jaribio la uhuru wa TAKUKURU kufanya kazi zake kwa mujibu wa sheria mpya ya k ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


CCM iache michezo ya Kitoto!

Mara baada ya Mheshimiwa Zitto kufungiwa kuhudhuria vikao vya Bunge, watu mbalimbali walitoa maoni yao. Mmoja kati ya watu hao ni Mbunge aliyeleta hoja ya kufungiwa Zitto Bungeni Mhe. Mudhihir Mudhihir (Mchinga , CCM). Katika makala yake aliyoandika kwenye gazeti la Mzalendo, Mhe. Mudhihir anafananisha mwitikio wa wananchi na mapokezi ya kishujaa anayoyapokea Zitto kuwa ni sawa na "Mchezo wa Kitoto". Makala yake hiyo unaweza kuisoma HAPA Na mimi niliamua kuandika kwenye gazeti jingine la K ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


"Sisi hatuogopi wala kumuonea haya mtu" - Mkurugenzi wa TAKUKURU

Nimepata nafasi ya kuzungumza na Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini, Bw. Edward Hosea. Licha ya matatizo kadhaa ya kiufundi, nimeweza hata hivyo kuwaletea sehemu ya mahojiano hayo. Natumaini hii itawapa mwanga juu ya majukumu na shughuli za taasisi hiyo nyeti katika kuendeleza utawala wa sheria nchini.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


"CCM wakitaka kuandamana wafanye, tunawangojea!" - Zitto

Ifuatayo basi ni sehemu ya pili na ya mwisho ya mahojiano yangu na Mbunge wa Kigoma Kaskazini Mhe. Zitto Kabwe. Leo anajibu kwa kina alichukuliaje majibu ya Malecela, na kuna mipango gani zaidi ya kuwahamasisha wananchi. Na wapinzani wanaitumia vipi fursa hii ili kujiimarisha? Na ana wito gani kwa wananchi ambao wameanza kuhamasika? Na maswali mengine mengi. Pichani mkutano wa Zitto Jangwani.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


"Mimi ni ishara ya Watanzania kuchoshwa" - Zitto akizunguma na KLH News

Nimepata nafasi ya kuzungumza na Naibu Katibu Mkuu wa Chadema na Mbunge wa Kigoma Kaskazini Mhe. Zitto Zuberi Kabwe. Katika mazungumzo yetu ambayo yamejadili sakata zima la yeye kusimamishwa vikao vya Bunge, Mhe. Zitto pia anazungumzia mwelekeo wa suala hili na mipango ya mbeleni ya kuzidi kuwaamsha Watanzania. Mahojiano yangu naye yamegawanyika sehemu mbili kutokana na urefu wake, na hivyo leo ninarusha sehemu ya kwanza ya mahojiano hayo leo, na sehemu ya pili itakuwa hewani mapema kesho. ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Breaking News! Kikwete azuiwa kuingia Buzwagi!

Wanakijiji wa maeneo yanayozunguka Buzwagi wamezuia msafara wa Rais Kikwete kuingia kwenye eneo ambalo Mgodi wa Buzwagi unatarajiwa kujengwa. Habari zaidi bila ya shaka tutazipata baadaye. Hata hivyo hapa nawaletea sehemu ya Hotuba ya Waziri Mkuu akilihairisha bunge. Bado ninapata matatizo na inaonekana si matatizo ya kompyuta yangu bali ni matatizo ya wao wenyewe podomatic.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


"Kilichofanyika ni kichekesho cha Demokrasia" - Dr. Slaa

Nimepata nafasi ya kuzungumza na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo na Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni Mhe. Dr. Wilbroad Slaa (Karatu) kuhusu kusimamishwa kwa Mhe. Zitto na pia kuhusu yeye kuondoa Bungeni hoja yake binafsi kuhusu Benki Kuu ya Tanzania. Sikupata muda wa kufanyia editing, mixing n.k kutokana na matatizo ya kompyuta za KLH News. Hivyo naweletea jinsi ilivyo, uncut, and unedited.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Kamati Teule yakataliwa - Zitto Apigwa Stop!

Mbunge machachari wa Kigoma Kaskazini Mhe. Zitto Kabwe (Chadema) ambaye aliamua kuleta hoja Bungeni ya kuundwa Kamati Teule ya Bunge ili kuchunguza jinsi Waziri wa Nishati na Madini Mhe. Nazir Karamagi alivyoweza kwenda Uingereza kutia sahini mkataba mpya wa uchimbaji wa madini kabla ya kumalizika upitiaji wa mikataba iliyopo kama ilivyoagizwa na Rais. Hoja hiyo inaonekana imewagawa wabunge kufuatana na itikadi za vyama vyao. Kubwa ambalo inaonekana kuwa limewaudhi baadhi ya wabunge ni ma ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Mabadiliko Bodi ya Mikopo - kutapatapa kwa Msolla?

Wote bila ya shaka mmeshasikia juu ya mswada wa vyombo vya habari, na sitashangaa kuwa mmewahi kusikia sheria mpya ya rushwa. Lakini ni wangapi wamesikia kuhusu mswada wa sheria ya mabadiliko ya Bodi ya Mikopo ya wanafunzi wa Elimu ya Juu? Ni wangapi wanajua kuwa mswada huo ulitangazwa kwenye gazeti la serikali mwezi Juni? Hakuna kitu kibaya kama serikali inayofanya mambo kisiri siri. Hatimaye, tunafahamu kuhusu mswada huo, na leo nachambua mapungufu yake na kunionesha ni jinsi gani kina Ms ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Kaboyonga Ambana Waziri Meghji kuhusu BOT!

Mapema leo Bungeni, Mbunge wa Tabora Mjini Mhe. Siraju Juma Kaboyonga alimbana Waziri wa Fedha Mhe. Zakia Meghji kuhusu gharama za ujenzi wa minara miwili ya benki kuu inayoendelea kujenga ambayo mpaka hivi sasa imegharibu mabilioni ya shiling. Majibu ya Waziri Meghji yamezua maswali mengi zaidi na inaonesha kuwa kuna kitu kinachoendelea. Pia ninawaletea hadithi yangu mpya iitwayo VIVIAN - PETE YA MACHOZI

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Inaudhi serikali inapojifanya mwalimu wa uandishi!

Wakati wa mjadala wa bajeti ya Wizara ya Habari, Michezo na Utamaduni jambo moja lilikuwa dhahiri. Wabunge wengi walijifanya wao ndio walimu wa waandishi wa habari kwa kutoa hoja ambazo bila ya shaka zilionsha upeo wao mdogo wa uhuru, haki, na ,majukumu ya vyombo vya habari. Hata wakati Waziri Mohammed Seif Khatib (Pichani) alipojumuisha hoja za wabunge na kutoa majibu ya maswali yao mbalimbalil alionekana mwenye kuzungumza kana kwamba serikali ndiyo pekee inayojua Uandishi ni fani ya namna ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Hoja za Uraia wa nchi mbili tuzikubali?

Kwa muda mrefu sasa mjadala wa uraia umekuwa ukiendelea nchini. Hoja hizo ambazo zinalengo la kubadili sheria ya Uraia nchini zimepata mtetezi mkubwa Bungeni ambaye ni Mbunge wa Singida Kaskazini Mhe. Lazalo Samuel Nyalandu (Pichani)ambaye kutokana na kuishi kwake nje ya nchi kwa muda mrefu ameweza kuwakakilisha mawazo ya watanzania wengi walioko ugenini ambao wanataka Tanzania ibadili sheria yake ya Uraia. Hata hivyo, je hoja zinazotolewa ni nzito kiasi cha kuweza kufanya Tanzania iruhusu ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Tanzania inahitaji Katiba Mpya au Mabadiliko tu ya Sheria?

Mjadala umefunguliwa, ili kujenga jamii yenye haki zaidi na usawa zaidi mbele ya sheria na kuwa na mfumo wenye usawa zaidi katika siasa za nchi yetu je, Tanzania tunahitaji Katiba Mpya au tufanye tu mabadiliko kwa kuzingatia mapendekezo ya Tume ya Jaji Nyalali na tume ya Jaji Kisanga.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


CCM iliahidi kutatua suala la Kadhi - Itaweza?

Jana Bungeni suala la mahakama ya kadhi mkuu wa Tanzania liliibuliwa tena katika jitihada za wapinzani kuitaka serikali ya CCM kutimiza ahadi yake ya kulitafutia ufumbuzi suala hilo kwa maislahi ya waislamu wa Tanzania. Je hoja zinazotolewa zinaridhisha? Je majibu yanayotolewa na serikali ya CCM yanatosheleza? Je kwa kuzingiatia mazingira ya Tanzania bara na katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania mahakama ya kadhi yaweza kuundwa bila kuleta mgongano wa kisheria au kimahusiano ya kidini? ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Wanafunzi Ukraine Kushitakiwa?

Kuna mambo mengi ya kuzungumza na kwa kifupi macho na masikio yangu yako Ukraine ambako vijana wetu wanakaribia kufikishwa mahakamani. Tafadhali tembelea http//www.jamboforums.com ambako utaona barua iliyotumika kuwaombea Visa toka Ubalozi wa Ukraine, na pia barua iliyotumwa wiki iliyopita ikiendelea kuwakana vijana hawa. Hivi kweli Tanzania tumefikia mahali ambapo kwa uzembe wa watu wachache tutaangalia vijana wetu wakisimamishwa mahakamani kwa kutaka kupata elimu tu?

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Bendera ya Taifa na KLH News International

Ndugu zangu ninazo bendera za taifa zipatazo 100 hivi (nimeshauza chache) na nataka kutumia kama sehemu ya jinsi ya kuchangia maendeleo ya KLH News. Bendera ninazigawa baada ya mchango wako wa kati ya dola 15-20 inategemea mahali ulipo. Unaweza kutumia paypal account, credit card, au debt card. Tafadhali ingia kwenye "PayPal - Your donation make this podcast possible" ili uweze kutuma. Ukishafanya hivyo nitumie email kuniambia kuwa mchango wako ni pamoja na kutaka kutumiwa bendera ili kutof ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Hatima ya waliokanwa Ukraine kujulikana leo?

Tafadhali tembelea tovuti hii kutwa nzima wakati tunafuatilia hotuba ya Waziri wa Sayansi, Teknolojia na Elimu ya Juu Mhe. Prof. Peter Msolla. Nina uhakika kuwa suala la vijana hawa kama halitakuwemo kwenye bajeti basi litakuwemo wakati wa majadililiano ya Bunge kama Kamati ambapo wabunge hupitia bajeti vifungu kwa vifungu. NI matumaini yangu kuwa leo jambo hilo litafikia mwisho wake kwa Bunge kuingilia kati na kuwaingiza vijana hawa kwenye bajeti ya mwaka huu na kuwafanya waendelee na maso ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


"Ni mapambano ya kifikra, lazima tushinde" - Mwanakijiji

Ndugu zangu mmegundua ni kitu gani kinaendelea Tanzania sasa hivi? Kutokana na kubadilisha hoja na mitazamo kunakofanyika sasa hivi Tanzania nina uhakika kuna mgongano wa kifikra unaoendelea. Ndugu zangu karibuni katika kutusaidia ili fikra za matumaini, usawa, na haki kwa wote zianze kushinda! (Picha ya yule mtu wa kale anayefikiria).

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Upotevu wa Mabilioni Benki Kuu, Mrema alisema kweli?

Madai ya upotevu wa mabilioni ya fedha toka Benki Kuu hayakuanza leo. Kwa wale wanaokumbuka watakumbuka kuwa madai ya upotevu wa mabilioni ya fedha ilikuwa ni mojawapo ya mambo ambayo yalimuengua Bw. Augustino Mrema toka serikali CCM na baadaye kujikuta akiwa upinzani Miezi michache kabla ya kuibuka tena kwa tuhuma za kupotea mabilioni ya fedha nilizungumza na Bw. Mrema kuhusu mambo mbalimbai yaliyokuwa yakimhusu yeye kisiasa na kiuongozi. Haya ni mahojiano yangu naye ambapo anatumia muda m ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Tuwaachie Nchi watawala wetu?

Tangu mtiririko wa kashfa uanze kuiandama serikali ya Tanzania hakuna hatua hata moja ya uhakika iliyochukuliwa kukabiliana na tuhuma hizo na hakuna mtu yeyote ambaye amewajibishw kwa kulisababisha Taifa hasara zisizo za lazima. Kuanzia kashfa kubwa ya Loliondo, IPTL, Ndege ya Rais, Tanesco, TTCL, KIA, Tanesco, Dawasa, Madini, Richmond, BOT na sasa Helikopta za kijeshi, serikali yetu imetia pamba masikioni kiasi cha kwamba haitaki kuambiwa wala kusikia. Hoja zinazotolewa Bungeni na wapinzan ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Machinjioni namna hii hadi nani afe!?

Hivi imekuwaje watanzania tumefikia mahali pa kuzoea ajali namna hii? Ndani ya wiki mbili ajalu nne zimetokea ambazo zimechukua maisha ya watu karibu 50 na watanzania tunaendelea na mambo yetu kama ajali hizo zimetokea sayari ya Zebaki! Kinachosikitisha zaidi ni kuwa Rais anapotuma rambirambi anawalaumu marehemu kwa kutopiga kelele vya kutosha kumkata dereva kwenda kasi! Hivi kwa mtindo huu kweli tutafika? Tufanye nini kuweza kupunguza ajali hizi zisizo za lazima? au ndio hivyo tena kilich ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Mhe. Anne Kilango na wanamapinduzi wasiobadilika!

Juzi Mbunge wa Same Mhe. Anne Kilango Malecela (Pichani) alizungumza Bungeni na kwa kutumia kauli kali alisema kuhusu jinsi serikali ilivyolegeza taratibu za ukaguzi wa makontena "Mimi nasema `No`, tutaimaliza nchi sasa". Jambo moja ambalo amelisahau ni kuwa CCM imeachana na mawazo ya kimapinduzi zamani na hawako tayari kujua kuwa tunaishi katika kipindi cha mabadiliko makubwa ya kizazi. Na ninyi mnaosikiliza matangazo haya mnaishi katika wakati muhimu na ambao si wa kujutia bali wa kutupa ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Twawapa Notisi watawala wetu! - Tanzania waliyoizoea...

Bunge hili halitakuwa kama mabunge mengine yaliyotangulia na huko tunakokwenda kutakuwa na mambo mengi zaidi ya kulifanya Bunge hili lichangamke na kuwajibika. Ni kwa sababu hiyo basi kitendo cha Dr. Slaa kuwasomea taarifa ya tuhuma ya umafia wa baadhi ya viongozi wetu ni kitendo ambacho kimewashtua watawala wetu na mshtuko huo ulijionesha kwa sura zao. Walipigwa na butwaa na mshangao kama watu waliojikuta wakinyeshewa na mvua na hapakuwa na pakukimbilia isipokuwa chini ya mwembe. Wakiwa ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Dr. Slaa Azua Bungeni suala la Mafia wa Tanzania!

Jana Bungeni, Mbunge wa Karatu Mhe. Wilbroad Slaa amezungumzia kuhusu ripoti ambayo imekuwa ikisambazwa kwenye mtandao kuhusu kundi la wahalifu wakimataifa ambao wamejikita katika utawala wa serikali na wameshirika vilivyo katika mikataba mbalimbali na masuala mbalimbali ambayo yameisababisha serikali yetu "kupoteza" mabilioni ya shilingi. Kama ripoti hiyo ina ukweli au la ni uamuzi wa msomaji mwenyewe. Vinginevyo, inawezekana kuwa amefungua kisanduku cha Pandora ambacho hawezi tena kukifun ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Umepata matumaini?

Waziri wa Fedha Mhe. Zakia Meghji (pichani) amewasilisha bungeni bajeti ya serikali ya mwaka 2007/2008. Bajeti hii ni ya makadirio ya mapato na matumizi ya serikali kwa mwaka huu mpya wa fedha. Wakati bajeti ya mwaka jana ilikuwa kali kwa wananchi na kwa vile ilikuwa ni bajeti ya kwanza ya utawala wa Rais Kikwete basi makosa ya hapa na pale na mapungufu ya hapa na pale yalitarajiwa. Mwaka mmoja baadaye matarajio ya watu yako juu zaidi kuwa Bajeti hii itakuwa ni ya kumpa nafuu mwananchi wa k ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Dr. Noordin Jella "Serikali iunde tume Huru"

Kati ya watu wote waliokwisha zungumzia suala hili la vijana Ukraine hakuna mwenye mtazamo wenye kutupa mwanga zaidi kama Dr. Noordin Jella. Yafuatayo ni mahojiano yangu naye na katika mahojiano hayo anapendekeza Rais aunde tume huru itakayochunguza ukweli wa jambo hili na kuhakikisha kuwa kama vijana hawa kweli walipewa mikopo na ilitakiwa iwafuate huko Ukraine wao wakitangulia, basi haki yao wapewe. Kama kuna makosa yalifanyika kati ya Dr. Jella au Wizara, vijana hawa wasiadhibiwe kwa "v ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Wabunge na Bunge "Lao"..

Bunge la Jamhuri linaanza kikao chake cha bajeti hivi karibuni. Kuna mambo kadhaa ambayo yanaendelea yanayolihusisha Bunge hili ambayo kwa kweli yanatufanya tujiulize kama kweli Bunge letu lina ubavu wa kuisimamia serikali au wajibu wake ni kujiongezea posho na marupurupu tu. - Kujiongezea posho ya mafuta ya shilingi milioni 480 kwa mwezi wa wabunge ni halali kweli? - Kufungia vyombo vya habari kwenye mikutano ya Kamati za Bunge, wanataka kuficha nini? nyongeza ya posho? - Kuacha serikali ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Exclusive: Mabinti Ukraine nao Wazungumza!

Tumeshawasikia kina kaka wakielezea hali yao huko Ukraine baada ya kutekelezwa na serikali. Je dada zao nao waliotelekezwa huko wanasemaje? Licha ya serikali kuwakana vijana hawa wote bado wanahitaji msaada wetu, msaada wa mtu yeyote mwenye mapenzi mema na anayewataki mema vijana hawa. Tafadhali ili kupata maelezo jinsi ya kuwasaidia: Bonyeza Hapa

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Why would President Kikwete Lie to the public?

It is sad and it should make us mad. Just like his subordinates did some few weeks ago, the President of Tanzania has decided to stick "with his men" and lie for them. For some of us who have been following up his public utterances, this however, is not the first time the president has knowingly or carelessly mislead the public. Why ain't we mad? Why people in Tanzania are so docile that they do not demand straight answers? Pichani Rais Kikwete, au Mfalme Kikwete?

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Ridhiwani achukua fomu.. CCM inatengenezeana njia?

Je kitendo cha watoto wa viongozi wa CCM kama kama kina Nape Nnauye, Zainab Kawawa, Vita Kawawa, Adam Malima, Hussein Mwinyi n.k kuanza kushika nafasi za uongozi katika CCM na kile cha kina Ridhiwani na wenzake kutaka kuingia kwenye nafasi hizo ni jambo ambalo watanzania waliangalie kwa hofu kwani CCM wameanza kurithishana vyeo au tuwaache vijana hawa watelekeze haki yao ya kikatiba na tusiwahukumu kwa makosa au matendo ya wazazi wao? Pichani Ridhiwani Kikwete akichukua fomu huku Bagamoyo, ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Prof. Mwandosya awakatalia wawekezaji Ngorongoro!

Kati ya vitu ambavyo hutokea mara chache Tanzania ni kitendo cha Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Profesa Mwandosha kumkatalia mwekezaji kujenga hoteli kwenye ukingo wa Crater ya Ngorongoro licha ya mamlaka nyingine husika kukubali mpango huo. Alichofanya Prof. Mwandosya kimenifanya nijiulize swali, hivi "kila anachotaka mwekezaji ni lazima apewe"? Je, kitendo hiki cha Mwandosha ni mfano wa mtu kujali nchi au ndio mazingaombwe yale yale?

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Mwenge wa Uhuru - Tuukimbize au tuukimbie?

Tangu kusimikwa juu ya mlima Kilimanjaro usiku ule wa kuamkia Uhuru, Watanzania tumeendelea kukimbiza mwenge huu kutukumbusha tunu hii iliyobora zaidi kwa mwanadamu, tunu iliyomfanya mtu mmoja kusema "nipe Uhuru au nipe Kifo". Hata hivyo kwa kadiri miaka inavyokwenda hatuna budi kujiuliza kama kweli ipo haja ya kukimbizana na moto huu au umefika wakati tuanze kuukimbia!! Pichani mwenge wa Uhuru ukiwa wilayani Karagwe, Kagera mwaka 2003

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Tuhuma dhidi Rais Mkapa: Ajibu asijibu?

Tangu kuondoka kwake madarakani Rais Mstaafu Ndg. Benjamin William Mkapa amekuwa akikabiliwa na tuhuma mbalimbali kuhusu utajiri alionao na hasa kuhusu baadhi ya matukio yaliyotokea wakati wa utawala wake. Hata hivyo, yeye mwenyewe hayuko tayari kujibu tuhuma hizo au hata kuonesha kuwa amezisikia na anazifanyia kazi. Swali ambalo bila ya shaka linawagawa Watanzania ni kama Rais Mkapa akae chini na kujibu tuhuma hizo au aendelee kuzipuuzia kuwa ni kelele za watu wenye wivu.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Watanzania mnaitwa, mtaitika? Serikali imekurupuka kujibu!

Serikali imetoa tamko lake na inaendelea kushikilia uzi ule ule wa kutowatambua vijana wetu waliokwama Ukraine. Hata hivyo, wakati umefika wa kuwasaidia vijana hawa kupitia akaunti iliyofunguliwa ili waendelee kusoma na si kurudishwa nyumbani wakiwa wameshindwa. Nimejibu hoja za serikali zilizotolewa jumatatu ambazo kwa kile zimeonesha hawakufuatilia suala hili kabisa na wamekurupuka tu kujibu kwa kusoma habari magazetini! Ili kuchangia hawa vijana tafadhali fuata maelekezo kama yanavyopat ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Flaviana, Ukraine, na Viongozi wetu!

Leo sitaki kusema mengi, kwani maneno mengi wakati mwingine huchosha. Hakikisha unampigia kura binti yetu Flaviana Matata. Why? pick any reason!

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Kikwete: "Kama (wizara) wangeshindwa wangeniambia!"

Hatimaye jana jumatano, ubalozi wa Uingereza kule Kiev, Ukraine umepata majibu toka Ubalozi wa Uingereza Tanzania ambao walikuwa wanafuatilia suala hili la vijana 29 waliokatishwa masomo yao baada ya serikali kushindwa kutimiza ahadi ya kuwasomesha. Jibu lililopatikana toka Wizara ya Sayansi, Teknolojia na Elimu ya juu ni kuwa serikali haiwatambui vijana hao, haihusiki kuwarudisha nyumbani na lolote litakalowapata ni shauri yao. Baada ya kuhakikisha jibu hilo na Ubalozi huo, nilijikuta sina ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Wanafunzi kujisalimisha Ubalozi wa Uingereza, Ukraine!

Wanafunzi wa kitanzania wapatao 29 waliotelekezwa na serikali ya Rais Jakaya Kikwete kwenye vyuo vya nchini Ukraine hatimaye wameamua kufanya kile walichotishia miezi michache iliyopita, nacho ni kujisalimisha na kuomba hifadhi kwenye Ubalozi wa Uingereza jijini Kiev, nchini Ukraine. Ubalozi huo tayari umeshakubali kuwapokea vijana hao mapema asubuhi. Uamuzi huo umefikiwa baada ya serikali ya Tanzania chini ya Wizara ya Sayansi na Elimu ya juu kuwakana wanafunzi hao na kutowatambua licha ya ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Halmashauri ya Taifa ya CCM ina uwezo huu?

Wiki iliyopita iliripotiwa na vyombo vya habari kuwa Chama cha Mapinduzi kupitia Halmashauri yake Kuu ya Taifa kitaanza kuwaita na kuwahoji watendaji wa serikali ili kuona kama wanatekeleza vyema Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2005-2010. Kwa nje nje jambo hilo halina tatizo lakini tukiliangalia kwa karibu tutaona kuwa kama litaachwa kusimama basi Tanzania tunaanza kurudi nyuma kwenye mtindo wa Chama Kimoja cha siasa na ni hatari kwa mgawanyo wa madaraka ulioanishwa vyema kikatiba. Pichan ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Msolla ajiuzulu

Leo namuondolea uvivu Prof. Msolla. Soma makala yangu kwenye Tanzania Daima.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Nakulilia Nchi Yangu!

Siwezi kusema mengi kuhusu hili, sikiliza wewe mwenyewe!!

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Wazazi wa wanafunzi Ukraine Wazungumza! Sehemu I

Nimezungumza na baadhi ya wazazi wa wanafunzi ambao leo hii bado wanapiga kambi kwenye ya ofisi za Ubalozi wa Uingereza Ukraine. Wanafunzi hao wamegoma kuondoka hapo hadi serikali iseme na kutatua tatizo lao. Wazazi nao mioyo yao imevunjika na wana ujumbe wa wazi kwa Rais Kikwete. Binafsi nimetoa mchango wangu kidogo wa kuwasaidia kwa chakula na matumizi hawa wanafunzi 20 hadi suala hili litatuliwe. Wakati tunasubiri serikali itatue (siyo kushughulikia) tatizo hili natoa wito tena muungane ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


TAKURU na Mkataba wa Richmond: Alichokwepa Hosea!

Wiki moja iliyopita, Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia Rushwa (TAKURU) Bw. Edward Hosea alitoa maamuzi kuhusu mkataba wa Richmond ambao serikali ya Rais Kikwete iliungia mwaka jana katika jitihada za kutafuta ahueni ya tatizo la nishati lililoikabili nchi yetu. Mkataba huu ulipoingiwa maswali mengi yaliulizwa na shutuma nyingi zilitolewa na mojawapo ya shutuma hizo ni kuwa kuna rushwa ilitumika. Bw. Hosea katika maelezo yake kwa vyombo vya habari alihitimisha mjadala huo kwa kusema kuwa "kati ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Wazazi wa wanafunzi wanazungumza Sehemu II

Ni maendelezo ya mazungumzo na wazazi wa vijana hawa.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Ya Zitto, Amina, na maadili ya ngono! asiye na dhambi..

Kama kile wabunge hawa wanachodaiwa kufanya ni kweli, je ndio mwisho wao kisiasa? Je vyama vyao viwachukulie hatua za kinidhamu, au bado wana nafasi nyingine?

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Vita vya Mawaridi - Una mbavu? shikilia...

Leo nawapa burudani ya kituko kimoja toka katika moja ya radio za hapa US. Natumaini itawapa weekend nzuri.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Dr. Hussein Mwinyi: "Muungano wetu ni wa Watu!"

Muungano wetu hatimaye umetimiza miaka 43. Licha ya misuko suko ya hapa na pale na migogoro ambayo ingeweza kabisa kutishia kuuvunja muungano huu, hata hivyo bado muungano unadumu na unaendelea kuwa nuru ya ndoto za waasisi wa Bara la Afrika la kuwa siku moja bara letu lingeweza kuungana. Muungano wetu ni muungano ambapo licha ya majaribio ya watu mbalimbali kujaribu kuudhofisha umeendelea kuwa imara na thabiti. Hata hivyo, kwa kadiri siku zinavyokwenda ndivyo tunavyoona jamii yetu na watu ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Bunge linapotukanwa tena!

Yafuatayo ni marudio ya matangazo niliyoyafanya mwaka jana baada ya Bunge kuambiwa kuwa haliwezi kupitia mikataba. Jambo hili limerudiwa tena na kwa vile mada ni ile ile basi badala ya mimi kurudia tena kuzungumzia hapa nimeona nirudie hili nililolisema wakati ule. Hata hivyo kuhusu hili la sasa nimeandika makala ambayo mtasoma siku ya Jumatano kuhusu suala hili. Picha ya ofisi ndogo ya Bunge, Zanzibar.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


"Mungu Usiwabariki viongozi wetu"!

Katika wimbo wa Taifa tunaimba na kuomba Mungu "wabariki viongozi wetu" itakuwaje kama tukianza kumuomba Mungu asiwabariki viongozi hao? Leo ninatoa sala na dua mbele ya Mwenyezi Mungu aache kuwabariki viongozi wetu, kwani kila walipobarikiwa, wamegeuza baraka hizo laana kwa nchi yetu!!

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Mapishi: "Mseto wa Samaki"

Nawatambulisha kwenu dada Mapenzi ambaye anawaletea maelekezo ya jinsi ya kupika mseto wa samaki. Tafuta kalamu na karatasi ili kuandika maelekezo ya mahitaji.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Zilipendwa - Usalama Jazz na Magereza!

Leo nimewaletea vibao vya 70s kutoka Polisi na Magereza. Natumaini vitawakumbusha mbali.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Mgomo Vyuo Vikuu - Prof. Msolla Wizara imemshindwa?

Hivi kwanini hii migomo inajirudia rudia. Aidha kuna uongozi mbovu kwenye wizara husika, au tumeshindwa kuwashawishi wanafunzi kuwa suluhisho la kudumula matatizo yao linaweza kupatikana. Vinginevyo, basi Watanzania ni watu wa ajabu sana kiasi cha kushindwa kushughulikia suala la elimu ya juu. Vyovyote vile, Prof. Peter Msolla anaendelea kuthibitisha kauli yangu ya huko nyuma kuwa kaishindwa wizara na anatutia aibu wasomi wenzake! Kwanini asing'atuke?

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Utawala wa Kikwete na Taifa la waliokata tamaa!?

Watanzania lazima tuangalie sana. Sasa hivi katika nchi yetu kuna hatari ya mamilioni ya watu kukata tamaa na kupoteza matumaini. Endapo tutafikia mahali (au kama tayari tumeshafikia) ambapo wananchi wa nchi hii watakata tamaa ya uongozi wao na kuamua "kila mtu na lwake" basi tujue kabisa hatima ya nchi yetu iko matatani. Picha ya watoto wa shule ya msingi, je hawa wakikata tamaa, Taifa lina hatima gani? Je Rais Kikwete anaweza kuturudishia matumaini kwa kizazi cha sasa na kijacho?

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Twamkumbuka Edward Sokoine - Mtu wa watu

Leo ni miaka 23 tangu Waziri Mkuu Edward Moringe Sokoine atutoke ghafla na kuacha simanzi na wingu la huzuni. Siku ile ya machozi na majonzi imebakia katika kumbukumbu za Watanzania wengi kama vile jana. Mfano wake ni kumbukumbu ya Wamarekani waliposikia habari za kuuawa kwa Rais John F. Kennedy. Kila mtu aliyekuwa mtu mzima wakati ule anakumbuka vizuri siku hiyo alikuwa wapi na alikuwa anafanya nini. Je pengo aliloliacha marehemu limeanza kuzibwa? Je kuna kiongozi yoyote ambaye anakaribi ...

Listen |