 Primary Format :
Also Listed as:
City : State/Province : Country : Country : User Tags:
User Votes:
RSS Feed Website
People found this Podcast
Searching for:
Tanzania News | news |
View this Podcast on a Google Map. 

Text Only listing of Sauti ya Mwanakijiji Podcasts
Trumix.com listings available of Sauti ya Mwanakijiji Podcasts
Click Here to Update the directory of this podcasts programs.
|
Trumix.com listings available of Sauti ya Mwanakijiji Podcasts
Build your own playlists with this podcast.
Rostam na Mtikila na kisa cha Milioni 3!
Mbunge wa Igunga Mhe. Rostam Aziz mapema leo amezungumza na waandishi wa habari akijibu kitendo cha Kanisa la KKKT kumkana na kutaka kumrudishia mchango alioutoa kusaidia Kwaya ya "Amkeni" ya Usharika wa Kinondoni. Katika majibu yake Bw. Rostam (CCM) ametoa madai makubwa pia likiwemo la kudai kuwa yeye amekuwa akisaidia makanisa na misikiti likiwemo Kanisa la Mchg. Christopher Mtikila.
Bw. Rostam amedai kuwa miezi mitatu iliyopita Mchg. Mtikila alienda kwake ... Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website Uhuru wa Taasisi zetu, kiini cha Utawala wa sheria!UCHUNGUZI WA BUNGE MFANO MBAYA WA UCHUNGUZI HURU
Jeshi la Polisi limetoa ripoti yake kuhusu uchunguzi wa kile kilichodaiwa vitendo vya kishirikina Bungeni karibu mwezi mmoja uliopita ambapo ilidaiwa mmojawapo wa wabunge alionekana akimwaga unga kwenye viti mbalimbali. Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma amesema kuwa (kati ya niliyoyanasa kwa haraka)
a. Hakuna Kamera iliyozimwa kuanzia mwaka 2006 (don't ask me walisema zilikuwa zimezimwa)
b. Kwenye mkanda uliodaiwa hakuna mtu aliyeonekana ... Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website Cheyo: "Serikali isilisingizie JWTZ kuhusu Meremeta"Mwishoni mwa juma nilipata nafasi ya kuzungumza na Mbunge wa Bariadi Mashariki Mhe. John Momose Cheyo (UDP) kuhusu suala la kampuni ya Meremeta ambayo imepokea mabilioni ya shilingi toka Benki Kuu na hakuna mtu aliye tayari kusema wazi kampuni hiyo ni ya nani.
Mahojiano yangu na Bw. Cheyo yalikuja masaa machacha baada ya majibizano yake na Waziri Mkuu Mhe. Pinda Bungeni siku ya Ijumaa ambapo alikataa kuyakubali maelezo ya Waziri Mkuu kuwa kampuni ya Meremeta na nyingine yenye kuhusiana naz ... Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website Chenge ahusishwa na Ushirikina!Tafadhali soma habari kamili kwenye http://www.klhnews.com Wakati huo huo tumeanza kutangaza "live" kama majaribio kwa kucheza muziki. Tunaomba feedback yako mahali popote unapotusikia na kama unatusikia vizuri, na hasa wale walioko Tanzania.Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website Leo ni Siku ya Bajeti - Jisomee kabla ya kusikia!Leo ni siku ya Bajeti. Waziri wa Fedha Bw. Mustafa Mkullo anatarajiwa kusoma bajeti hiyo leo na hivyo kuonesha ni wapi tumefika toka mwaka uliopita na wapi tunataka kwenda katika mwaka ujao wa fedha.
Nimepata nafasi ya kupata nakala ya bajeti hiyo ambayo inapatikana hapa: http://www.jamiiforums.com/attachment.php?attachmentid=1680&d=1213211256
Tafadhali copy and paste kwenye browser yako.
Nimatumaini yangu mtapata nafasi ya kuipitia kabla hamjaisikia.
Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website Huu si wakati wa kukata tamaa! Bila ya shaka mlolongo wa matukio kadha wa kadha unaweza kumfanya mtu yeyote kushika tama na kukata tamaa. Hasa inapotokea matukio ambayo yanaihusu nchi yetu. Msururu wa kashfa ambazo zimeiandama nchi na viongozi wetu bila ya shaka vinaweza kukufanya ujisikie mpweke na mnyonge na zaidi kuweza kujiuliza "Tanzania ina matatizo gani?".
Kwa wengine kujiuliza swali hili kunaendana na hisia ya kuachwa peke (abandonment) na kukata tamaa (despair). Na zaidi ya yote kuna wengine ambao wanaweza kuj ... Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website Exclusive: Mhe. Anne Kilango Malecela azungumza na KLHNTulikokuwa tunaenda siko, tumeamua kugeuka" - hayo ni baadhi ya maneno ya Mhe. Anne Kilango Malecela akizungumza na KLH News siku chache zilizopita akielezea mabadiliko ya wabunge wa CCM linapokuja suala la kulinda maslahi ya Taifa.
Kati ya mambo ambayo anayazungumzia ni pamoja na hali ya kisiasa nchini, kifo cha Ballali, kwanini wabunge wa CCM walikuwa wanaitetea serikali yao hata ilipokuwa inaharibu, kwanini anaamini Kikwete ni kweli anataka mabadiliko na ... Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website Wabunge wahoji kifo cha BallaliHii ni marudio ya show tuliyofanya siku ya Jumapili. NI sehemu tu ya onesho hilo. Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website Gov. Balali Afariki DuniaAliyewahi kuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania Dr. Daud Balali amefariki dunia. Habari ambazo zimeanza kusikika tangu jana jioni na kuthibitishwa na ndugu zake zimesema kuwa Gavana Balali amefariki mwishoni mwa juma na mipango ya mazishi inafanywa. Anatarajiwa kuzikwa huko huko Marekani. Inatarajiwa taarifa ya kifo chake kutangazwa Tanzania baadaye leo. Sikiliza matangazo kuhusu kifo hicho hapa au kwa kutwa nzima ya kesho tutakuwa tunaleta maendeleo yoyote ya habari hii kwenye tovuti yetu y ... Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website Alichozungumza Mhe Zitto Detroit! Karibu wiki moja iliyopita Mhe. Zitto Kabwe alizungumza na jumuiya ya Watanzania waishio Jimbo la Michigan nchini Marekani. Mazungumzo hayo yaliyofanyika wakati wa hafla ya chakula cha jioni aliyoandaliwa Bw. Zitto yaligusia mambo mbalimbali na hasa kuwataarifu wanajumuiya hiyo mambo mbalimbali yanayoendelea nyumbani na pia kusikiliza maoni na maswali yao.
Matangazo ya leo basi ni hotuba ya Mhe. Zitto kwa jumuiya hiyo na sehemu ya maswali na majibu, yote ni uncut and an edited. Makosa meng ... Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website Nimevunja Mwiko - Soma "Kulikoni" la LeoKwa karibu wiki mbili sasa nimekuwa nikitengeneza hoja na kumulika kama vile kurunzi idara ya Usalama wa Taifa. Sikiliza introduction ya makala yangu maalum kwenye gazeti la "Kulikoni" leo. Kwa wale ambao hampo nyumbani makala hii itawekwa baadaye mchana wa Ijumaa (saa za Marekani) kwenye http://www.klhnews.com upande wa editorial. Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website Chenge - mbona anatuchengua!?Chenge ni bilionea wa kutupwa ambaye kwake shilingi Bilioni moja anayodaiwa kuificha huko Marekani ni sawa na "vijisenti" vichache. Hivi tatizo letu liko wapi? Je yawezekena kuwa chenge ni dalili tu ya tatizo? Je eye ni kiongozi pekee wa TAnzania ambaye amewekeza mabilioni ya shilingi kwenye akaunti za kigeni? Je ajiuzulu au na yeye anaweza akalia kuwa amefanywa "Bangusilo" wa rada!? Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website KLH Exclusive: "Mafuriko Kyela - 40,000 hatarini!" - Dr. Harrison MwakyembePichani baadhi ya wananchi wakijaribu kuvuka mto. Kidaraja hicho sasa hakipitiki tena. Picha kwa hisani ya Mjengwa
Mvua za masika zimezidi kupamba moto nchini na zimekuwa zikisababisha mafuriko sehemu mbalimbali. Baadhi ya maeneo ambayo yamepata mafuriko ni pamoja na Vunjo, Same na Kyela. Hata hivyo hadi hivi sasa ni wilaya ya Kyela ambayo ina kata 15 ambazo kati ya hizo 11 zimepatwa na mafuriko makubwa .
Siku ya Jumamosi nimepata nafasi ya kuzungumza na Mbunge wa Jimbo la Kyela Dr. Harr ... Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website Bila CCM Madhubuti? - Mwalimu alisema kweli...Mwanzoni sikuyaelewa maneno ya Baba wa Taifa Mwl. J.K. Nyerere kuwa “Bila CCM Madhubuti nchi yetu itayumba”. Nilifirikia kuwa alimaanisha “Bila CCM” nchi yetu itayumba, na pia nilidhania alimaanisha kuwa “Bila viongozi wa CCM” nchi yetu itayumba. Miaka hii ilivyopita na hasa baada ya matukio yaliyolikumba Taifa letu ndio maana hasa ya maneno yake imeanza kuniingia na kwa hakika nimekubali kuwa bila Chama cha Mapinduzi ambacho ni “madhubuti” basi Taifa letu liko matatani, na ... Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website Operesheni Demokrasia Comoro - Wangwe angekaa kimya!Saa na wakati huu vikosi vya majeshi ya Jumuiya ya Afrika vimeanza mapambano ya kukikomboa kisiwa cha Anjouan ili hatimaye kurudi katika shirikisho la Comoro. Vikosi hivyo vikiongozwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania wanashiriki katika Operesheni Demokrasia Komoro yenye lengo la kumuondoa Rais aliyejipachika Bw. Mohammed Bacar.
Hivyo saa na wakati kama huu ambapo vijana wetu wako katika hali ya hatari na ambapo wanayaweka maisha yao hatarini ni kitendo cha kutokuwajibika kwa mwanasiasa kam ... Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website Sisi tumepotea wapi?Ndugu zangu, mlolongo wa matukio ambayo yameliandama Taifa letu kwa miaka kadhaa sasa na ambayo kilele chake bado hatujui kitafikia lini yanathibitisha jambo moja kubwa, kwamba sisi kama Taifa kuna mahali tumekwenda kombo. Kuna mahali ambapo sisi kama taifa tumepotea njia na hatuko tayari kukubali kuwa tumepotea na matokeo yake tumeendelea kufuata njia ile ile ya upotevu tukiamini kuwa huko mbeleni mambo yatanyoka.
Je, Tanzania tunayoiona leo hii, ndiyo hii ambayo tuliitaka na ambayo waze ... Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website Walioiba EPA wasiepe Pingu! Habari za kuwa wale walioifanya uhalifu kwenye akaunti ya EPA wameanza kurudisha fedha zile zimepokelewa kwa hisia zinazopingana. Kuna wale ambao wanaona uamuzi huo ni wa kupongeza kuwa "angalau fedha zinarudi" na hawa wanasema kuwa baada ya fedha kurudi ndiyo tufuatilie suala la kupelekwa wahalifu hawa mahakamani.
Kuna wale wengine ambao wanaamini kuwa fedha kurudishwa kungeenda sambamba na wahalifu kuchukuliwa hatua za kisheria badala ya ilivyo sasa. Watu hawa nikiwemo mimi naamini tun ... Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website Mahojiano na DCI : "Jambo Forums haihusiani na Ughaidi"Baada ya msemaji wa Jeshi la Polisi kuihusisha Jambo Forums na Ughaidi niliamua kutafuta msimamo wa wale wanaochunguza ili watuambie kweli wana amini kuwa JF inahusiana na Ughaidi.
Nilipata nafasi ya kuzungumza na Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DCI) Kamanda Robert Manumba na kumuuliza mambo kadhaa yanayohusiana na Jambo Forums na kukamatwa kwa wawili kati ya wanachama wake kama 4000.
Tafadhali karibu usikilize mahojiano hayo na kwa habarii za kutwa nzima usikose kuingia http://www.klhnew ... Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website Jambo Forums na Ughaidi?Jana ilikuwa ni siku ya huzuni katika jitihada za kupanua uhuru wa habari na maoni Tanzania; jeshi la Polisi lilikiri kuwa linawashikilia watu wawili kutokana na kuhusika kwao na JF kwa madai kuwa tovuti hiyo inahusiana na uchochezi na mambo ya Kighaidi.
Inasikitisha kuona kuwa Jeshi letu la Polisi badala ya kuwakamata watu waliokwapua fedha za umma na ambao wameliingizia Taifa letu hasara limeamua kuwatafuta watu walioufunua ufisadi hadharani. Hili limesikitisha sana. Ni kwa sababu hiyo w ... Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website Mizengo Pinda Waziri Mkuu mteulePichani Waziri Mkuu Mteule Bw. Mizengo Pinda akipongezwa na wabunge mara baada ya kulipitisha jina lake kuwa Waziri Mkuu
Rais Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Mhe. Mizengo Pinda (Mpanda Mashariki) kuwa Waziri Mkuu mpya kuchukua nafasi ya Mhe. Edward Lowassa aliyejiuzulu kufuatia kashfa ya Richmond.
KLH News international inakuletea taarifa ya uteuzi huo hapa kwenye podomatic na pia kwenye http://www.klhnews.com ambapo tunafuatilia maendeleo ya sakata hili linalojifunua kila baada ya masaa ... Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website Lowassa aandika barua ya kujiuzulu- JK atakubali?Tafadhali sikiliza maoni yangu kuhusu hili. Na zaidi ya yote hakikisha unatembelea KLH News through out the day for any breaking news and for any new development kufuatia kashfa hii ya Richmond. Ukienda kwenye "Archives" hapa utaweza kusikiliza mahojiano yangu na Dr. Mwakyembe miezi michache iliyopita.
Pichani Mbunge wa Kyela - CCM na Mwenyekiti wa Kamati iliyochunguza Richmond Mhe. Dr. Harrison Mwakyembe akitopewa mkono wa pongezi (pole?) na wabunge wenzake. Picha kwa hisani ya Mroki Mro ... Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website Wabunge wanaokurupuka, na Kampeni za KitetoLeo hii vichwa vya habari vya magazeti mengi nyumbani vinahusu jinsi wabunge walivyodai ripoti kamili ya uchunguzi wa BoT badala ya maelezo ya juu yaliyotolewa na Waziri wa Fedha Bi. Zakia Meghji Bungeni jana.
Binafsi siyo tu nasikia kinyaa lakini nakerwa na wabunge ambao kama watu walioamshwa usingizini wanakurupuka na kuanza kujifanya ati leo wamekuwa watetezi wa BoT
Wabunge hawa walikuwa wapi wakati wa miaka 15 ya ufisadi kwenye benki yetu Kuu? Walikuwa wapi wakati Meremeta na ndugu za ... Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website Tumepigwa ganzi ya Ufisadi?Mlolongo wa kashfa umeigubika serikali ya Tanzania na kama vile watu wanashindana imekuwa ni kashfa juu ya kashfa.
Swali ambalo linanisumbua hasa baada ya kashfa ya BoT naona watu wamekuwa kama wametiwa ganzi ya aina fulani, kuwa hatusikii tena uchungu na tumekubali kuwa "mambo ndivyo yalivyo"
Je tukubali kuwa tuko katika utamaduni wa kifisadi na mambo ndivyo yalivyo? Je tukubali kuwa sisi sote ni mafisadi wa aina moja au nyingine na tukipewa nafasi hizo walizonazo wao bila ya shaka na ... Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website Mahojiano na Waziri wa Fedha Bi. Zakia Meghji (MB)Je, Bi. Zakia Meghji naye ni fisadi? Je kitendo chake cha kuandika barua kuthibitisha malipo kwa kampuni iliyotajwa kwenye ripoti ya BoT na baadaye kuikana barua hiyo baada ya kufahamu ukweli ni kitendo cha kifisadi? Je, anapaswa kujiuzulu?
Nimezungumza na waziri wetu wa fedha kujaribu kutafuta baadhi ya majibu ya maswali hayo. Sikiliiza na uamue mwenyewe. Kama huwezi kusikiliza hapa kwa sababu yeyote ile, unaweza kusikiliza mahojiano haya kwenye http://www.klhnews.com eneo la podcast pal ... Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website Ripoti ya Kamati Teule kuhusu Richmond, wananchi wasubiri! Hatimaye Ripoti ya uchunguzi kuhusu kampuni ya Richmond Development ya Houston imekamilika na hatimaye kukabidhiwa rasmi kwa Spika wa Jamhuri ya Muungano hapo jana na Mwenyekiti wa Kamati Teule ya Bunge Dr. Harrison Mwakyembe (Kyela - CCM) pichani.
Kamati hiyo imetumia siku 45, mashahidi 75, vielelezo zaidi ya mia moja na maswali zaidi ya 2700. Kwa kifupi ni kuwa ukilinganisha na uchunguzi wa PCCB inawezekana wananchi watataka Kamati Teule ifanye uchunguzi wa mambo mengine yote kuliko Taas ... Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website Heri ya Krismasi !Wapendwa wasikilizaji kwa niaba yangu na ya KLH News napenda kuwatakia ndugu zetu Wakristu mahali pote duniani na wengine wote heri ya Krismasi wanapoadhimisha kuzaliwa kwa Mkombozi Bwana Yesu Kristu. Kutoka hapa kijijini na kwenu nyote nawatakia heri ya Krismasi. Mnayoisikiliza ni kwaya ya Vijana ya Kanisa Katoliki la Mtakatifu Theresa Arusha mjini. Albamu yao inatoka hivi karibuni na bila ya shaka kwa watakaopenda wanaweza kuwasiliana nami kuona jinsi gani wataweza kuinunua. Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website Eid Mubarak!Napenda kutumia nafasi hii kuwatakia heri ya siku kuu ya Eid ndugu zetu waislamu wanapoungana na na Waislamu wengine katika kuunganisha mioyo yao katika kuhitimisha mojawapo ya Nguzo za Uislamu, yaani Hijja. Tunapowafikiria wale waliokuwa wamekwama uwanja wa ndege tuna matumaini kuwa serikali imefanya mipango mizuri na ya uhakika ili kuweza kuwarudisha wote salama na bila ya usumbufu wowote ule. Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website Mahojiano na Jaji Mark Bomani wa Kamati ya MadiniYafuatayo ni mahojiano yangu na Jaji Mark Bomani, Mwenyekiti wa Kamati ya Ushauri ya Rais kuhusu Sekta ya Madini. Nilipata nafasi ya kuzungumza naye kuhusu kamati hiyo na majukumu yake. Majibu ya Jaji Makani yanaweza kuwashangaza watu wengi. Zaidi ya yote miaka 46 baada ya Uhuru; wapi tulipo, wapi tunataka kwenda. (Pichani, Amir Jamal, Dereck Brycson, JK Nyerere, Chief Abdallah Fundikira, Gorge Kahama
Nyuma: Kushoto Solomon Eliofoo, Rashid Kawawa, Nsilo Swai, Oscar Kambona, Tewa Saidi Tew ... Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website Mkapa na Yona wanyang'anywe Kiwira?Wakiwa madarakani Rais Benjamini Mkapa na Waziri wake wa Nishati na Madini waliingia ubia na kuanzisha kampuni ya Tanpower Resources. Wakati Yona analiambia Bunge kuwa wanatafuta wawekezaji wa "kufufua" Mgodi wa Makaa ya Mawe wa Kiwira, sirini walikuwa wanapanga yeye na Rais wake kuwa "wawekezaji" hao watakuwa ni wao wawili. Na miezi michache kabla Rais Mkapa hajaachia madaraka, Mgodi wa Kiwira ulikuwa chini ya viongozi hao wawili wakiwa na hisa zaidi ya asilimia 80. Hadi leo hii hakuna ali ... Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website Buriani mzee Kanyama Chiume... Most of us knew his name by reading his articles and opinions in Mzalendo, Daily News and Uhuru; He was one of the leading nationalists of his time and indeed a patriot of Africa, a true son of our beloved motherland. Mr. Chiume who was born in Malawi and later exiled to Tanzania was a "leader of Nyasaland African Congress and served as the Minister of Education and the Minister for Foreign Affairs in the 1960s." according to one popular website. Beside writing for Tanzania Newspaper he als ... Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website Salamu kwa Siku ya Wanafunzi Duniani - Ukumbi wa DDCLeo kama mnavyofahamu kulikuwa na makongamano ya wanafunzi jijini Dar-es-Salaam. Moja lilifanyika Ukumbi wa Ubungo Plaza na kuhutubiwa na Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Mhe. Pius Msekwa na lile jingine lililofanyika Ukumbi wa DDC na kuhutubiwa na wasomi mbalimbali na viongozi wa chama cha Demokrasia na Maendeleo akiwemo Mhe. Zitto Kabwe. Nilipata nafasi ya kutuma salamu za mshikamano kwa kongamano la DDC baada ya kuombwa kutuma ujumbe huko. Walioko nyumbani waliupata kwa njia ya maandishi, ... Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website Tuwakatalie watawala wetu?Wakati umeanza kufika ambapo wananchi waanze kuwakatalia watawala wao!! Nisikilize leo nikifafanua kwanini tuanze kuwakatalia na ni vitu gani hivyo vya kukataa! Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website Hongera Mheshimiwa Spika..... WATANZANIA hatuna budi kupiga vigelegele, makofi na hoihoi za shangwe! Hatuna budi kucheza mdundiko, lizombe, gita, mganda, na mdumange! Hatuna budi kutunga tenzi, ngonjera na nyimbo za sifa kwani Spika wetu, amevaa vazi lenye michirizi ya dhahabu lililochirizwa Ulaya!
Kuna wakati hatuna budi kuondoa tofauti zetu za kisiasa, na hasa wivu usio na msingi, hasa tunapoona mwenzetu amefanikiwa. Si tu kuziondoa na kuziweka pembeni tofauti hizo, bali hata kuzizika na kuzisahau kabisa hasa inapoto ... Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website ~ * ~ The Spoken Word - "I Can't Wait" ~ * ~ By. M. M. mwanakijiji
Wondering, and hoping, and praying
That it’ll all be alright!
That my country will rise and be
A nation, and it will take its place among the nations
Of the World and it’ll be a rightful place.
But our rulers keep telling us, just wait!
]They tell us to wait,
When we ask about corruption,
And when we question their intentions
They come back with political intimidation
That if we don’t stop, there’ll be a confrontation,
So they tell us people! just wait!
... Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website KLH Exclusive: Mahojiano na Dr. Salim Ahmed SalimTarehe 14 Oktoba 2007 ni miaka nane kamili, tangu Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere atutoke na kutuacha wakiwa. Kati ya viongozi na watanzania wachache waliopata kumfahamu Mwalimu kwa karibu na kuwa wasaidizi wake wa karibu ni Dr. Salim A. Salim ambaye aliwahi kushika nafasi mbalimbali za uongozi katika serikali ya Zanzibar na baadaye katika serikali ya Muungano.
Baadhi ya nafasi ambazo aliwahi kushika ni pamoja na Ubalozi, Uwaziri (akiwa Waziri Mkuu, Waziri wa Mambo ya Nchi ... Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website Eid Mubarak kwenu Nyote!!! Napenda kutumia nafasi hii kuwatakia ndugu zetu Waislamu wa Tanzania wanapoungana na Waislamu wengine pote duniani kuadhimisha siku kuu hii ya Eid el Fitr wanapomalizia mfungo Mtukufu wa Ramadhani. Siku ya Jumapili tunatarajia kuwa na matangazo "live" kupitia Bongoradio.com tunapoadhimisha miaka nane tangu Baba wa Taifa atutoke. Hivyo usikose matangazo hayo kuanzia kama saa nane mchana EST sawa na saa tatu za Usiku EAT.
Kwa wale Wakristu na watu wa imani nyingine nawakaribisha kwenye ukura ... Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website Nyerere: " Ikulu ni Mzigo, kwanini wanakukimbilia?"Hii ni sehemu ya pili ya Hotuba ya Mwalimu Mei Mosi 1995. Hapa ndipo alipokuwa mwiba wa serikali ya CCM hasa baada ya kudai kuwa wameacha "Mambo ya Msingi" . Ni katika sehemu hii lile swali muhimu la "kuna biashara gani Ikulu" liliulizwa. NImefanya editing zaidi kidogo ya kupunguza sauti za watu uwanjani ili mwalimu asikike vizuri na ningekuwa na muda zaidi kidogo ningefanya bora zaidi, mniwie radhi kwa mwangwi kidogo.Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website Nyerere Mei Mosi '95: "Watanzania Mjomba wenu ni nani?"Ifuatayo ni sehemu ya kwanza ya hotuba aliyoitoa Baba wa Taifa kwenye sherehe za Mei Mosi 1995. Tunapokumbuka miaka nane tangu Mwalimu Nyerere afariki hatuna budi kupitia japo kwa hatua hazina ya hekima yake.
Wakati anatoa hotuba hii mwaka 1994 kulikuwa na mgomo wa wafanyakazi, na mwaka 1995 ulikuwa ni mwaka wa uchaguzi na huo ukiwa ni uchaguzi wa kwanza baada ya kurejesha tena mfumo wa vyama vingi. Hivyo, Mwalimu alipokuwa anatoa hotuba hii watu wengi walikuwa wanaonesha nia ya kutaka kw ... Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website Mhe. Moh'd Seif Khatib: "Viongozi hawazomewi, ni uongo!"Siku ya Jumamosi kwenye matangazo yetu ya moja kwa moja (live) nilipata nafasi ya kuzungumza na Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo wa Serikali ya Tanzania Mhe. Mohammed Seif Khatib (MB).
Makubwa tuliyozungumza ni suala zima la tuhuma zilizotolewa na ushirika wa wapinzani tarehe 15 Septemba pale Jijini Dar. Pamoja na hayo tulizungumzia kuhusu suala la Buzwagi na jinsi mwitikio wa wananchi ulivyokuwa na hasa ziara ambazo zimefanywa wiki iliyopita na Mawaziri na Manaibu wao kwenye mikoa ... Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website "Majibu ya serikali hayatoshelezi" - Mahojiano na Tundu LissuSiku ya Jumamosi nilipata nafasi ya kuzungumza kwa kirefu na mwanaharakati wa mazingira na mwanasheria wa Chadema ambaye pia ni Wakili katika Mahakama Kuu ya Tanzania Bw. Tundu Lissu. Katika mazungumzo yetu ambayo yalirushwa moja kwa moja (live) kupitia Bongoradio.com tulizungumzia madai ya wapinzani na mkataba wa Buzwagi ambao Bw. Lissu ndiye aliuchambua hadharani kwenye kipindi cha "Jenerali on Mondays". Mahojiano haya ni karibu saa nzima. Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website CCM ikubali tatizo kwanza...!! Tangia sakala la "orodha ya ufisadi" lianze, serikali ya CCM imekuwa ikitoa majibu ya kukanganyana na mengine hayaingii akili hata kidogo. Majibu mengine yamejaa kiburi na dharau na mengine inabidi mtu ajiulize "walikuwa wanafikiria nini".
Kwa maoni yangu kabla ya viongozi wa serikali na wa CCM kuanza kutoa majibu kuhusu tuhuma kwa viongozi 11, la kwanza ambalo wangelifanya ni kukubali tatizo kwanza, hiki kiburi wanachokionesha kuwa wao hawawezi kukosea na wengine wanadai kuwa wamekuwa w ... Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website Nini kimemsibu Jaji Warioba?Kama ripoti iliyoandikwa na gazeti la Habari Leo ina ukweli basi kuna kitu kinachoendelea na ambacho bila ya shaka kimemsibu Jaji Warioba kuja na mawazo ya aina hii. Hebu soma na uamue mwenyewe au ni mimi ndiyo nimechanganyikiwa.
[b]Mgaya Kingoba
HabariLeo; Friday,September 28, 2007 @00:02[/b]
WAZIRI Mkuu mstaafu, Jaji Joseph Warioba amesema amekerwa na tabia ya wanasiasa kupakana matope na kuonya kuwa kisingizio cha utawala bora kisitumiwe kutaka kuangusha dola zilizopo madarakani.
“T ... Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website Tundu Lissu auchambua Mkataba wa BuzwagiNInawaletea mahojiano ya Mwanasheria maarufu nchini anayeshughulika na Haki za Binadamu na Masuala ya Mazingira na pia anayefuatilia masuala ya madini Bw. Tundu LIssu. Mahojiano hayo yalirushwa moja kwa moja na Channel Ten na kwa msaada wa mtazamaji CMB wa Jambo Forums tunaweza kuyaletea hapa mahojiano hayo. Sikiliza kwa makini na uamue. Pia tunajitahidi kupata nakala ya mkataba huo. Kwa wale walioko nyumbani mnaweza kusoma juu ya Mkataba huo kwenye magazeti ya "This Day" na "Kulikoni" na b ... Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website CCM isipuuzie hoja za Wapinzani, wazijibu!Uongozi wa Chama cha Mapinduzi umeamua kuwa hoja zilizotolewa na watanzania kuhusu masuala mbalimbali hazistahili kujibiwa. Kwa mujibu wa Katibu wa Idara ya Uenezi na Itikadi ya Chama hicho Mhe. Aggrey Mwanri MB (CCM - Siha) CCM haitaenda mahakamani bali itaenda kwa wananchi na kujibu hoja za watanzania hao kwa kuwataka wananchi wazipuuze hoja hizo. Miongoni mwa hoja ambazo Mhe. Mwanri anataka wananchi wazipuuzie ni zile zile za Ubadhirifu wa Benki Kuu, Mikataba ya Madini hususan ule wa Buz ... Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website Rais Mkapa na Matumizi mabaya ya Ikulu - Dr. Slaa Ifuatayo ni sehemu ya pili ya mahojiano yangu Dr. Slaa kufuatia mkutano wao mkubwa uliofanyika mwishoni mwa wiki. Nimeambatanisha pia orodha na maelezo mliyoyasikia kwenye mahojiano haya ili uweze kupitia moja baada ya nyingine na uweze kutolea maamuzi wewe mwenyewe. Bonyeza Hapa KudownloadListen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website Kukamatwa wabunge wa CCM, Ishara ya Nyakati?Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa imewatia mbaroni viongozi kadhaa wa Chama cha Mapinduzi kwa tuhuma za kujihusisha na vitendo vya rushwa. Miongoni mwao ni wabunge Michael Laizer wa Longido na Elisa Mollel wa Arumeru Mashariki. Hii ni mara ya kwanza katika miaka ya hivi karibuni kuwa Chama cha Mapinduzi kiko tayari kuwatosha baadhi ya viongozi wake wakubwa. Je inawezekana huu ni mwanzo wa nyakati mpya na ni jaribio la uhuru wa TAKUKURU kufanya kazi zake kwa mujibu wa sheria mpya ya k ... Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website CCM iache michezo ya Kitoto!Mara baada ya Mheshimiwa Zitto kufungiwa kuhudhuria vikao vya Bunge, watu mbalimbali walitoa maoni yao. Mmoja kati ya watu hao ni Mbunge aliyeleta hoja ya kufungiwa Zitto Bungeni Mhe. Mudhihir Mudhihir (Mchinga , CCM). Katika makala yake aliyoandika kwenye gazeti la Mzalendo, Mhe. Mudhihir anafananisha mwitikio wa wananchi na mapokezi ya kishujaa anayoyapokea Zitto kuwa ni sawa na "Mchezo wa Kitoto". Makala yake hiyo unaweza kuisoma HAPA Na mimi niliamua kuandika kwenye gazeti jingine la K ... Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website "Sisi hatuogopi wala kumuonea haya mtu" - Mkurugenzi wa TAKUKURUNimepata nafasi ya kuzungumza na Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini, Bw. Edward Hosea. Licha ya matatizo kadhaa ya kiufundi, nimeweza hata hivyo kuwaletea sehemu ya mahojiano hayo. Natumaini hii itawapa mwanga juu ya majukumu na shughuli za taasisi hiyo nyeti katika kuendeleza utawala wa sheria nchini. Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website "CCM wakitaka kuandamana wafanye, tunawangojea!" - ZittoIfuatayo basi ni sehemu ya pili na ya mwisho ya mahojiano yangu na Mbunge wa Kigoma Kaskazini Mhe. Zitto Kabwe. Leo anajibu kwa kina alichukuliaje majibu ya Malecela, na kuna mipango gani zaidi ya kuwahamasisha wananchi. Na wapinzani wanaitumia vipi fursa hii ili kujiimarisha? Na ana wito gani kwa wananchi ambao wameanza kuhamasika? Na maswali mengine mengi. Pichani mkutano wa Zitto Jangwani. Listen | Listen in your iPhone | Download | |