Search for Podcasts
Podcast
Internet Radio

Podcast Directory:
Browse Podcasts
Add your Podcast
Remove a Podcast
Search for Podcasts
Podcast Directory
by Country
by Language
by Buzz
by Popularity
by Category
by Tags
by Region
by City
on a Google Map



Podcast Help:
What is Podcasting
Creating an XML
Podcast Hosting
Podcast Software
Firefox Plugin
Podcast Hardware




About Us:
Podcast Advertising
Contact Us
Copyright Issues
Help Wanted



Running and Fitness

Run Saturday


Internet Radio:
Find
State
Country
Language
Music
Sports
Regions
Popularity

Trumix.com
Our New Site
Internet Radio
Podcasts
Create a Playlist



Discount Gold Offer

Sauti ya Mwanakijiji Podcasts

PodcastDirectory / News and Politics / News
PodcastDirectory / Regions / AF / Tanzania

Primary Format :
News

Language :
Kiswahili

Also Listed as:

City :
Mwanza
State/Province :
Unknown
Country :
Tanzania
Region :
AF
User Tags:

User Votes:

RSS Feed
Website

People found this Podcast

Searching for:

View this Podcast on a Google Map.

Podcast iTunes Link

Text Only listing of Sauti ya Mwanakijiji Podcasts

Methings.com listings of Sauti ya Mwanakijiji Podcasts

If you like this podcast, you might also like:

CCM matatani; Upinzani Mashakani - ngoma 2010!

Sijui kama kweli tunataka mabadiliko au tunaombea mabadiliko yatokee. Sijui kama tunafanya ili kusababisha mabadiliko au tunasubiri wengine wafanye ili tufurahie mabadiliko; Sijui hata kama tunajua vizuri ni mabadiliko gani hasa tunayataka na kama tunataka ni juhudi gani tumezifanya kushiriki kwenye mchakato wa kuleta mabadiliko hayo. Tunaweza kubishana vijiweni na kwenye mitandao na kujaribu kubadilishana mawazo mchana kutwa na usiku kucha lakini mabadiliko hayaji kwa kusema. Mabadiliko h ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Ripoti juu ya Meremeta yatoka

Unaweza kupata sneak ripoti hiyo kwenye http://www.mwanakijiji.com Password ya kufungulia Ripoti Sneek Pek: meremeta1997 Inapatikana hivi: (Tafadhali angalia masahihisho kutoka taarifa yetu ya Ijumaa) Ripoti inapatikana kwa njia ya pre-ordering (yaani order zikishatimia zote zinatolewa kwa wakati mmoja) kwa wale ambao watachangia dola 30 au shilingi elfu thelathini tu au zaidi kwa njia zifuatazo: * Kupitia Mtandao wa http://www.mwanakijiji.com kuna kitufye cha kuchangia upande wa kul ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Ziara ya Dowans HQ in Costa Rica na Meremeta

Hi everyone; I'm back, wounded and limping but still kicking LOL. With some of my "little ones" we were able to travel extensively through Europe, US and Costa Rica as well as making some contacts in Singapore, U.A.E (this was published in one of previous Cheche editions. What we have discovered is nothing less than shocking! I visited the so called Headquarters of Dowans S.A in Costa Rica and had access to relevant organs that deal with businesses there. Some of the things we were abl ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Taarifa ya Habari Juni 10, 2009

Ifuatayo ni taarifa ya habari ya saa mbili za Usiku Juni 10, 2009 kwenye TBC

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Uvamizi na Uharibifu Arumeru: Mahojiano na Mhe. Kimaro

Kwa usiku kucha kundi la wahuni waliojibatiza jina la "wanakijiji" na kutuchafua wengine walivamia eneo la Mhe. Aloyce Kimaro (Vunjo-CCM) na kuharibu mazao na kuchoma nyumba na kuiba mali mbalimbali, walifanya hivyo kwa kile ambacho gazeti la Mwananchi limeelezea kuwa "wanadai kwamba, kwa kuwa shamba hilo liko katika eneo lao wangepewa ili walitumie kwa shughuli mbalimbali ikiwemo kujenga shule, hivyo kitendo cha serikali kuliuza kwa mtu wa nje ya kijiji hicho ni kunyanganya haki yao." Kit ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Maoni yangu Juu ya Busanda kwenye Star TV

Siku ya Jumamosi nilialikwa kuwa mmoja wa wachangiaji katika kipindi cha "Tulonge Asubuhi" kinachorushwa na Star TV Jijini Mwanza. Mada kuu ilikuwa tulilojifunza kutokana na Uchaguzi mdogo wa Busanda. Wachangiaji wengine ambao nao walipata nafasi ya kuchangia kwenye onesho hilo la asubuhi ni pamoja na Erasto Tumbo (Chadema), na Amos Makalla (CCM) pamoja na wapiga simu wengine. Ni matumaini nitaendelea kupata nafasi kama hii ili kuendelea kuchochea mabadiliko ya kifikra ambayo mara zote ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Kule tulikotoka, ndiko kule kwa Chinova?

Unaweza kusikiliza kwa kudownload kutoka hapa au kusikiliza moja kwa moja kwa kubonyeza "play" chini hapa. http://www.box.net/shared/qfp38sfr3n Ukisikiliza usiniulize, na wala usimwambie mtu mwingine. For your Ears Alone! M.M.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Uongozi na Maendeleo: - Sauti kutoka Ahera

Ningeweza kukuambia kilichomo lakini sitakutendea haki; itabidi usikilize mwenyewe.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Nani ashinde, nani ataamua mshindi?

Ni mgongano wa kihistoria ambao ulipaswa kutokea. Ni mgongano ambao hutokea mahali popote panapokuwa na tofauti kubwa kati ya watawala na watawaliwa. Ndivyo ilivyokuwa kwenye Mapinduzi ya Ufaransa, Mapinduzi ya Marekani na Mapinduzi ya Bolshevik (Urusi). Ni yale yale yaliyotokea na kusababisha mapinduzi ya Cuba yaliyomuingiza Castro madarakani. Ndiyo! Ni yale yale yaliyotokea pia kwenye mapinduzi ya Zanzibar! Migongano ya namna hiyo asili yake mara zote ni pale wananchi wanapotambua kuwa ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Mlipuko 511KJ Mbagala: Majanga na kuishi kwa kudra!

Kwa namna fulani tunaamini kuwa sisi tuna upendeleo wa aina fulani kwa Mwenyezi Mungu, kwamba nchi yetu kwa sababu upendeleo wa pekee basi haitapata majanga. Hatujajifunza kwa ajali zinazotea mara kwa mara za mabasi, hatujajifunza kwenye ajali za majini, hatujajifunza kwenye milipuko ya mabomu na kwa hakika tuko kama tumepigwa ganzi ya aina fulani hivi. Pamoja na kutoa pole na rambirambi, ni lazima tujiulize tutaendelea mpaka kulini kwa kutegemea rehema za Mungu? Sitoshangaa leo tutaambiw ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Mahojiano na Mhe. Lucas Selelii (Nzega) - "Mmekula hamshibi?"

Salaam, Tumepata nafasi ya kuzungumza kwa kirefu na Mhe. Lucas Selelii Mbunge wa Nzega, miongoni mwa wabunge wenye msimamo wa kimabadiliko na miongoni mwa vinara wa vita dhidi ya ufisadi ndani ya CCM na katika Taifa. Tafadhali hakikisha unasoma sehemu ya ahadi yetu kwani tuna ujumbe muhimu kwa wasomaji wetu na wanachama wetu. Ungana nasi pia kwenye mijadala motomoto kwenye forum yetu ya http://www.mwanakijiji.com ambapo mojawapo ya mijadala ya kina ni suala la Rais wa zamani Mzee Ally Ha ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Mahojiano na Mhe. William Ngeleja kuhusu Dowans

Mpango wa serikali kutaka kuyanunua majenereta ya kuzalisha umeme ambayo yaliletwa nchini na Kampuni ya Dowans katika mkataba wake na kampuni feki iliyoumbuliwa ya Richmond hautokani na kulazimika kufanya hivyo bali hali halisi ya hali ya nishati nchini ndiyo inalazimisha serikali kupanga kuchukua hatua hiyo. Hayo yamesemwa na Waziri wa Nishati na Madini Mhe. William Ngeleja alipozungumza na tovuti hii hapo jana kuelezea kile ambacho kinaonekana mgongano wa kimtazamo kati ya Wizara, kamati ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Kwanini Masha bado Waziri?

Natamani ningeweza kusema kwa nguvu ninachosema kisema hapa. Natamani ningekuwa na sauti kubwa zaidi kuweza kusikika kuhusu mauaji ya Leticia Bahati siku tatu zilizopita. Ninachojiuliza ni kwanini Masha bado ni Waziri wa Mambo ya Ndani? Lakini kuna maswali makubwa zaidi ya hilo ambayo ninayauliza leo kwenye "Nguvu ya Hoja"! Sikiliza.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Pinda aangusha kilio, akwepa kujibu swali!

Waziri Mkuu Mhe. Mizengo Pinda ametumia nafasi yake ya kujibu maswali Bungeni kugusa hisia za wabunge kwa kuonesha uchungu uliomgusa kufuatia mauaji ya maalbino ambayo yamekuwa yakiendelea nchini. WM Pinda alimwaga machozi hayo baada ya kuulizwa kuhusu kufafanua kauli yake iliyotaka watu watakaoshukiwa au kutuhumiwa mauaji ya albino na wao kuuawa hapo hapo. Alipoulizwa kwanini ahalalishe mauaji hayo na kwanini atoe kauli zinazonesha kukikanzina na utawala wa sheria na Katiba ambao ni msin ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Mwakyembe aunguruma "Mashtaka yanayoletwa ni mepesi"

Mbunge wa Kyela na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM Mhe. Dr. Harrison Mwakyembe amesema kuwa mashtaka mbalimbali yanayoletwa hivi sasa dhidi ya watuhumiwa mbalimbali wa ufisadi bado ni "mepesi" na anatajia kuwa baada ya uchunguzi kufanyika zaidi mashtaka hayo yatabadilishwa na kuwa mazito yakiwemo yale ya sheria ya Uhujumu uchumi.Hayo na mengine mengi ameyasema katika mahojiano yake na KLHN ya mwanakijiji.com ambayo yalirushwa moja kwa moja siku ya Jumapili. Unaweza kuyasikiliza ma ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Utetezi wangu wa Sofia Simba

Nikiri ya kwamba nimesikitishwa na kushangazwa sana na baadhi ya ukosoaji wa Mhe. Simba kufuatia mahojiano yangu naye siku chache zilizopita. Kilichonisikitisha zaidi ni jinsi gani baadhi yetu tuna angalia vitu ambavyo si vya msingi na kuviacha vya msingi; kilichonishangaza zaidi ni jinsi gani wengine wamekuwa wa kali kiasi cha wao wenyewe kuwa kile wanachomtuhumu Mhe. Simba.. arrogance! Katika mahojiano yangu na watu mbalimbali (kama Dr. Migiro, Dr. Salim, na wengineo) sijawahi kujaribu ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Mahojiano na Mhe. Sofia Simba

Mojawapo ya chaguzi ambazo zimekuwa na mvuto wa muda mrefu ndani ya CCM ni ule uliofanyika mwishoni mwa juma lililopita ambapo Mwenyekiti mpya wa Jumuiya ya Wanawake wa CCM (T) alipatikana. Mshindi huyo si mwingine bali Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mhe. Sofia Simba. Safari ya ushindi wake ilikuwa ni safari ambayo wachache wako tayari kuipitia. Ilikuwa ni safari ambayo unapofika mwisho inabidi ujiuliza ulianzaje safari hiyo. Hivyo KLHN ilipata nafasi ya kuzungumza naye kwa kirefu kuhusu ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Exclusive: Dr. Slaa azungumzia yaliyojiri Mbeya Vijijini

Mwishoni mwa mwaka jana nilipata nafasi ya kuzungumza na Bongoradio.com kuhusu masuala mbalimbali ya kufunga mwaka. Ninawaletea sehemu kidogo ya mahojiano hayo pamoja na mahojiano niliyoyafanya na Mhe. Dr. Wilbroad Slaa (Karatu-Chadema) kuhusu kilichosababisha mgombea wao msomi mwanasheria Bw. Sambwee Shitambala kushindwa kufuata taratibu rahisi za kuapa kabla ya kushirki uchaguzi huo mdogo. Baada ya kusikiliza mahojiano hayo piga kura na upande wa kulia wa tovuti hii na utoe maoni yako ni ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Mwaka 2008: Mwaka watawala walipopigishwa magoti!

Mwaka wa 2008 ndiyo huo umefikia ukingoni. Na pamoja nao ni matamu na machungu yote, furaha na huzuni, kicheko na kilio! Ni mwaka ambao umeweka historia nyingi katika nchi yetu na nje ya nchi! Hata hivyo ya nchi nyingine tutawaachia wengine, lakini kwetu sisi wenyewe tunaweza kusema pasipo shaka yoyote ile kuwa mwaka huu ulioisha ni mwaka ambapo watawala walipigishwa magoti na watawaliwa! Jinsi gani unaweza kuuliza; sikiliza tafakari yangu ya kufunga mwaka 2008. Nakutakia wewe na vyote ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Tutaka kujitawala au tulibadilisha watawala?

Tulipodai haki yetu ya kuwa watu huru tulidai ili baadaye kiwe nini? Tulipoona fahari bendera ya Ufalme wa Uingereza ikiteremka taratibu usiku ule wa kukumbukwa na ya Tanganyika huru ikapindishwa tulikuwa tuna njozi ya aina gani ya Taifa? Siku ile wazee wetu walipocheza kwa furaha na kushangilia kuwa "na sisi ni huru" walikuwa wanafurahia uhuru hasa kutoka kitu nani na kwa nini? Je yawezekana kile tulichoshangilia wakati ule, miaka 47 iliyopita sicho ambacho tunacho leo hii? Je njozi zile ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Julius Mtatiro azungumzia kukamatwa na Polisi kwa Uchochezi!

Mara baada ya kupata dhamana katika kesi yake ya uchochezi iliyofunguliwa mjini Dar, Bw. Julius Mtatiro alipata nafasi ya kuzungumza nasi kupitia KLHN kwa kirefu kuhusu sakata zima la kukamatwa kwake na madai mbalimbali yaliyozunguka tukio la kukamatwa na muda aliokuwa mikononi mwa Polisi. Je ni kweli aliteswa, Je alikataliwa mwanasheria, na je anahusika vipi na migomo inayoendelea kiasi cha kufunguliwa mashtaka mazito kama haya? Sikiliza majibu kupitia MWANAKIJIJI.COM au KLHN (site zote m ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Remembering Mama Africa Miriam Makeba - Malaika

South African singing legend and activist "Mama Africa" Miriam Makeba's great grandchild Lindelane (L) says farewell to her after her coffin arrived at Johannesburg's OR Tambo Airport from Italy, where she died age 76. South African President Kgalema Motlanthe on Wednesday declared a period of national mourning for music legend and anti-apartheid activist Makeba. (AFP/DFA/Jacoline Prinsloo) Join us at: http://www.mwanakijiji.com

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Taarifa ya Maendeleo ya msiba wa Ndali Nzaro

Kwa heshima kubwa na Taadhima wana Familia ya Nzaro waliopo Detroit Michigan wakiongozwa na Da Mboja Nzaro na Mwamvita Nzaro pamoja na rafiki wa kike wa Marehemu Saada Ali, wanapenda kutoa shukrani za dhati kabisa kwa niaba ya familia nzima ya Nzaro iliyoko nyumbani Tanzania pamoja na jamaa na ndugu wote kwa mwitikio mkubwa kutoka sehemu mbalimbali wa rambirambi, maneno ya faraja na misaada ya hali na mali iliyotolewa mpaka sasa. Tunashukuru vyombo mbalimbali vya habari na hasa mitandao mb ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Serikali yaipiga mkwara Mwanahalisi, Kubenea ajibu hoja!

Kwenye ukurasa wa mbele kuna habari iliyozua kasheshe Tanzania. Habari hii ilitoka kwenye gazeti la Mwanahalisi la Jumatano la kupokelewa kwake kumekuwa na hisia za aina yake kwani siku ya pili yake Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo iliandika barua kwa Mwanahalisi kutaka maelezo juu ya habari hiyo ambayo kwa maoni ya serikali inaonekana ni kiuchochezi na kiuchonganishi. Watu wa serikali wanaona kuwa habari hiyo ilikuwa na lengo la kumchonganisha Rais na viongozi wenzake wa CCM hasa Mhe ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Juu ya vifo vya Watoto 20 Tabora, siku ya Idi Mosi.

Bila ya shaka utakuwa umeshasikia na kugushwa na habari za vifo vya watoto wapatao ishirini waliokuwa siku ya Idi huko Tabora kwenye ukumbi wa Muziki kutokana na kukosa hewa na kukanyagana wakitafuta kutoka ukumbini humo. Hii ni sehemu ya kwanza ya maoni yangu, sehemu ya pili itakuwa kwenye gazeti siku ya Jumapili. Ni lazima tukasirike.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Mahojiano na Nape Nnauye kuhusu kusimamishwa Uanachama

Nape Nnauye ni mgombea wa nafasi ya Uenyekiti wa Taifa wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM). Nafasi hiyo inagombewa na vijana wengine 27. Miezi michache iliyopoita Bw. Nnauye alianzisha mjadala mkubwa pale alipodai hadharani kuwa taratibu za kuingia mkataba wa Jengo la Umoja wa vijana zilikiukwa na mkataba wenye haukuwa na faida kwa umoja wa vijana. Akasema hadharani kuwa aliyewahi kuwa Waziri Mkuu Bw. Edward Lowassa pamoja na Uongozi wa Umoja huo akiwemo Mwenyekiti wa sasa Bw. Nchi ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Cheche mitaani Septemba 2

Toleo jipya la "Cheche za Fikra" liko mitaani. Jipatie nakala yako kupitia http://www.klhnews.com

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Leo ni Siku ya Bajeti - Jisomee kabla ya kusikia!

Leo ni siku ya Bajeti. Waziri wa Fedha Bw. Mustafa Mkullo anatarajiwa kusoma bajeti hiyo leo na hivyo kuonesha ni wapi tumefika toka mwaka uliopita na wapi tunataka kwenda katika mwaka ujao wa fedha. Nimepata nafasi ya kupata nakala ya bajeti hiyo ambayo inapatikana hapa: http://www.jamiiforums.com/attachment.php?attachmentid=1680&d=1213211256 Tafadhali copy and paste kwenye browser yako. Nimatumaini yangu mtapata nafasi ya kuipitia kabla hamjaisikia.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Huu si wakati wa kukata tamaa!

Bila ya shaka mlolongo wa matukio kadha wa kadha unaweza kumfanya mtu yeyote kushika tama na kukata tamaa. Hasa inapotokea matukio ambayo yanaihusu nchi yetu. Msururu wa kashfa ambazo zimeiandama nchi na viongozi wetu bila ya shaka vinaweza kukufanya ujisikie mpweke na mnyonge na zaidi kuweza kujiuliza "Tanzania ina matatizo gani?". Kwa wengine kujiuliza swali hili kunaendana na hisia ya kuachwa peke (abandonment) na kukata tamaa (despair). Na zaidi ya yote kuna wengine ambao wanaweza kuj ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Exclusive: Mhe. Anne Kilango Malecela azungumza na KLHN

Tulikokuwa tunaenda siko, tumeamua kugeuka" - hayo ni baadhi ya maneno ya Mhe. Anne Kilango Malecela akizungumza na KLH News siku chache zilizopita akielezea mabadiliko ya wabunge wa CCM linapokuja suala la kulinda maslahi ya Taifa. Kati ya mambo ambayo anayazungumzia ni pamoja na hali ya kisiasa nchini, kifo cha Ballali, kwanini wabunge wa CCM walikuwa wanaitetea serikali yao hata ilipokuwa inaharibu, kwanini anaamini Kikwete ni kweli anataka mabadiliko na ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Gov. Balali Afariki Dunia

Aliyewahi kuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania Dr. Daud Balali amefariki dunia. Habari ambazo zimeanza kusikika tangu jana jioni na kuthibitishwa na ndugu zake zimesema kuwa Gavana Balali amefariki mwishoni mwa juma na mipango ya mazishi inafanywa. Anatarajiwa kuzikwa huko huko Marekani. Inatarajiwa taarifa ya kifo chake kutangazwa Tanzania baadaye leo. Sikiliza matangazo kuhusu kifo hicho hapa au kwa kutwa nzima ya kesho tutakuwa tunaleta maendeleo yoyote ya habari hii kwenye tovuti yetu y ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Alichozungumza Mhe Zitto Detroit!

Karibu wiki moja iliyopita Mhe. Zitto Kabwe alizungumza na jumuiya ya Watanzania waishio Jimbo la Michigan nchini Marekani. Mazungumzo hayo yaliyofanyika wakati wa hafla ya chakula cha jioni aliyoandaliwa Bw. Zitto yaligusia mambo mbalimbali na hasa kuwataarifu wanajumuiya hiyo mambo mbalimbali yanayoendelea nyumbani na pia kusikiliza maoni na maswali yao. Matangazo ya leo basi ni hotuba ya Mhe. Zitto kwa jumuiya hiyo na sehemu ya maswali na majibu, yote ni uncut and an edited. Makosa meng ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Nimevunja Mwiko - Soma "Kulikoni" la Leo

Kwa karibu wiki mbili sasa nimekuwa nikitengeneza hoja na kumulika kama vile kurunzi idara ya Usalama wa Taifa. Sikiliza introduction ya makala yangu maalum kwenye gazeti la "Kulikoni" leo. Kwa wale ambao hampo nyumbani makala hii itawekwa baadaye mchana wa Ijumaa (saa za Marekani) kwenye http://www.klhnews.com upande wa editorial.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Chenge - mbona anatuchengua!?

Chenge ni bilionea wa kutupwa ambaye kwake shilingi Bilioni moja anayodaiwa kuificha huko Marekani ni sawa na "vijisenti" vichache. Hivi tatizo letu liko wapi? Je yawezekena kuwa chenge ni dalili tu ya tatizo? Je eye ni kiongozi pekee wa TAnzania ambaye amewekeza mabilioni ya shilingi kwenye akaunti za kigeni? Je ajiuzulu au na yeye anaweza akalia kuwa amefanywa "Bangusilo" wa rada!?

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


KLH Exclusive: "Mafuriko Kyela - 40,000 hatarini!" - Dr. Harrison Mwakyembe

Pichani baadhi ya wananchi wakijaribu kuvuka mto. Kidaraja hicho sasa hakipitiki tena. Picha kwa hisani ya Mjengwa Mvua za masika zimezidi kupamba moto nchini na zimekuwa zikisababisha mafuriko sehemu mbalimbali. Baadhi ya maeneo ambayo yamepata mafuriko ni pamoja na Vunjo, Same na Kyela. Hata hivyo hadi hivi sasa ni wilaya ya Kyela ambayo ina kata 15 ambazo kati ya hizo 11 zimepatwa na mafuriko makubwa . Siku ya Jumamosi nimepata nafasi ya kuzungumza na Mbunge wa Jimbo la Kyela Dr. Harr ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Bila CCM Madhubuti? - Mwalimu alisema kweli...

Mwanzoni sikuyaelewa maneno ya Baba wa Taifa Mwl. J.K. Nyerere kuwa “Bila CCM Madhubuti nchi yetu itayumba”. Nilifirikia kuwa alimaanisha “Bila CCM” nchi yetu itayumba, na pia nilidhania alimaanisha kuwa “Bila viongozi wa CCM” nchi yetu itayumba. Miaka hii ilivyopita na hasa baada ya matukio yaliyolikumba Taifa letu ndio maana hasa ya maneno yake imeanza kuniingia na kwa hakika nimekubali kuwa bila Chama cha Mapinduzi ambacho ni “madhubuti” basi Taifa letu liko matatani, na kwa hakika lita ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Operesheni Demokrasia Comoro - Wangwe angekaa kimya!

Saa na wakati huu vikosi vya majeshi ya Jumuiya ya Afrika vimeanza mapambano ya kukikomboa kisiwa cha Anjouan ili hatimaye kurudi katika shirikisho la Comoro. Vikosi hivyo vikiongozwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania wanashiriki katika Operesheni Demokrasia Komoro yenye lengo la kumuondoa Rais aliyejipachika Bw. Mohammed Bacar. Hivyo saa na wakati kama huu ambapo vijana wetu wako katika hali ya hatari na ambapo wanayaweka maisha yao hatarini ni kitendo cha kutokuwajibika kwa mwanasiasa kam ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Sisi tumepotea wapi?

Ndugu zangu, mlolongo wa matukio ambayo yameliandama Taifa letu kwa miaka kadhaa sasa na ambayo kilele chake bado hatujui kitafikia lini yanathibitisha jambo moja kubwa, kwamba sisi kama Taifa kuna mahali tumekwenda kombo. Kuna mahali ambapo sisi kama taifa tumepotea njia na hatuko tayari kukubali kuwa tumepotea na matokeo yake tumeendelea kufuata njia ile ile ya upotevu tukiamini kuwa huko mbeleni mambo yatanyoka. Je, Tanzania tunayoiona leo hii, ndiyo hii ambayo tuliitaka na ambayo waze ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Walioiba EPA wasiepe Pingu!

Habari za kuwa wale walioifanya uhalifu kwenye akaunti ya EPA wameanza kurudisha fedha zile zimepokelewa kwa hisia zinazopingana. Kuna wale ambao wanaona uamuzi huo ni wa kupongeza kuwa "angalau fedha zinarudi" na hawa wanasema kuwa baada ya fedha kurudi ndiyo tufuatilie suala la kupelekwa wahalifu hawa mahakamani. Kuna wale wengine ambao wanaamini kuwa fedha kurudishwa kungeenda sambamba na wahalifu kuchukuliwa hatua za kisheria badala ya ilivyo sasa. Watu hawa nikiwemo mimi naamini tun ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Mahojiano na DCI : "Jambo Forums haihusiani na Ughaidi"

Baada ya msemaji wa Jeshi la Polisi kuihusisha Jambo Forums na Ughaidi niliamua kutafuta msimamo wa wale wanaochunguza ili watuambie kweli wana amini kuwa JF inahusiana na Ughaidi. Nilipata nafasi ya kuzungumza na Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DCI) Kamanda Robert Manumba na kumuuliza mambo kadhaa yanayohusiana na Jambo Forums na kukamatwa kwa wawili kati ya wanachama wake kama 4000. Tafadhali karibu usikilize mahojiano hayo na kwa habarii za kutwa nzima usikose kuingia http://www.klhnew ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Jambo Forums na Ughaidi?

Jana ilikuwa ni siku ya huzuni katika jitihada za kupanua uhuru wa habari na maoni Tanzania; jeshi la Polisi lilikiri kuwa linawashikilia watu wawili kutokana na kuhusika kwao na JF kwa madai kuwa tovuti hiyo inahusiana na uchochezi na mambo ya Kighaidi. Inasikitisha kuona kuwa Jeshi letu la Polisi badala ya kuwakamata watu waliokwapua fedha za umma na ambao wameliingizia Taifa letu hasara limeamua kuwatafuta watu walioufunua ufisadi hadharani. Hili limesikitisha sana. Ni kwa sababu hiyo w ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Mizengo Pinda Waziri Mkuu mteule

Pichani Waziri Mkuu Mteule Bw. Mizengo Pinda akipongezwa na wabunge mara baada ya kulipitisha jina lake kuwa Waziri Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Mhe. Mizengo Pinda (Mpanda Mashariki) kuwa Waziri Mkuu mpya kuchukua nafasi ya Mhe. Edward Lowassa aliyejiuzulu kufuatia kashfa ya Richmond. KLH News international inakuletea taarifa ya uteuzi huo hapa kwenye podomatic na pia kwenye http://www.klhnews.com ambapo tunafuatilia maendeleo ya sakata hili linalojifunua kila baada ya masaa ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Lowassa aandika barua ya kujiuzulu- JK atakubali?

Tafadhali sikiliza maoni yangu kuhusu hili. Na zaidi ya yote hakikisha unatembelea KLH News through out the day for any breaking news and for any new development kufuatia kashfa hii ya Richmond. Ukienda kwenye "Archives" hapa utaweza kusikiliza mahojiano yangu na Dr. Mwakyembe miezi michache iliyopita. Pichani Mbunge wa Kyela - CCM na Mwenyekiti wa Kamati iliyochunguza Richmond Mhe. Dr. Harrison Mwakyembe akitopewa mkono wa pongezi (pole?) na wabunge wenzake. Picha kwa hisani ya Mroki Mro ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Wabunge wanaokurupuka, na Kampeni za Kiteto

Leo hii vichwa vya habari vya magazeti mengi nyumbani vinahusu jinsi wabunge walivyodai ripoti kamili ya uchunguzi wa BoT badala ya maelezo ya juu yaliyotolewa na Waziri wa Fedha Bi. Zakia Meghji Bungeni jana. Binafsi siyo tu nasikia kinyaa lakini nakerwa na wabunge ambao kama watu walioamshwa usingizini wanakurupuka na kuanza kujifanya ati leo wamekuwa watetezi wa BoT Wabunge hawa walikuwa wapi wakati wa miaka 15 ya ufisadi kwenye benki yetu Kuu? Walikuwa wapi wakati Meremeta na ndugu za ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Tumepigwa ganzi ya Ufisadi?

Mlolongo wa kashfa umeigubika serikali ya Tanzania na kama vile watu wanashindana imekuwa ni kashfa juu ya kashfa. Swali ambalo linanisumbua hasa baada ya kashfa ya BoT naona watu wamekuwa kama wametiwa ganzi ya aina fulani, kuwa hatusikii tena uchungu na tumekubali kuwa "mambo ndivyo yalivyo" Je tukubali kuwa tuko katika utamaduni wa kifisadi na mambo ndivyo yalivyo? Je tukubali kuwa sisi sote ni mafisadi wa aina moja au nyingine na tukipewa nafasi hizo walizonazo wao bila ya shaka na ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Mahojiano na Waziri wa Fedha Bi. Zakia Meghji (MB)

Je, Bi. Zakia Meghji naye ni fisadi? Je kitendo chake cha kuandika barua kuthibitisha malipo kwa kampuni iliyotajwa kwenye ripoti ya BoT na baadaye kuikana barua hiyo baada ya kufahamu ukweli ni kitendo cha kifisadi? Je, anapaswa kujiuzulu? Nimezungumza na waziri wetu wa fedha kujaribu kutafuta baadhi ya majibu ya maswali hayo. Sikiliiza na uamue mwenyewe. Kama huwezi kusikiliza hapa kwa sababu yeyote ile, unaweza kusikiliza mahojiano haya kwenye http://www.klhnews.com eneo la podcast pal ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Ripoti ya Kamati Teule kuhusu Richmond, wananchi wasubiri!

Hatimaye Ripoti ya uchunguzi kuhusu kampuni ya Richmond Development ya Houston imekamilika na hatimaye kukabidhiwa rasmi kwa Spika wa Jamhuri ya Muungano hapo jana na Mwenyekiti wa Kamati Teule ya Bunge Dr. Harrison Mwakyembe (Kyela - CCM) pichani. Kamati hiyo imetumia siku 45, mashahidi 75, vielelezo zaidi ya mia moja na maswali zaidi ya 2700. Kwa kifupi ni kuwa ukilinganisha na uchunguzi wa PCCB inawezekana wananchi watataka Kamati Teule ifanye uchunguzi wa mambo mengine yote kuliko Taas ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Heri ya Krismasi !

Wapendwa wasikilizaji kwa niaba yangu na ya KLH News napenda kuwatakia ndugu zetu Wakristu mahali pote duniani na wengine wote heri ya Krismasi wanapoadhimisha kuzaliwa kwa Mkombozi Bwana Yesu Kristu. Kutoka hapa kijijini na kwenu nyote nawatakia heri ya Krismasi. Mnayoisikiliza ni kwaya ya Vijana ya Kanisa Katoliki la Mtakatifu Theresa Arusha mjini. Albamu yao inatoka hivi karibuni na bila ya shaka kwa watakaopenda wanaweza kuwasiliana nami kuona jinsi gani wataweza kuinunua.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Eid Mubarak!

Napenda kutumia nafasi hii kuwatakia heri ya siku kuu ya Eid ndugu zetu waislamu wanapoungana na na Waislamu wengine katika kuunganisha mioyo yao katika kuhitimisha mojawapo ya Nguzo za Uislamu, yaani Hijja. Tunapowafikiria wale waliokuwa wamekwama uwanja wa ndege tuna matumaini kuwa serikali imefanya mipango mizuri na ya uhakika ili kuweza kuwarudisha wote salama na bila ya usumbufu wowote ule.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Mahojiano na Jaji Mark Bomani wa Kamati ya Madini

Yafuatayo ni mahojiano yangu na Jaji Mark Bomani, Mwenyekiti wa Kamati ya Ushauri ya Rais kuhusu Sekta ya Madini. Nilipata nafasi ya kuzungumza naye kuhusu kamati hiyo na majukumu yake. Majibu ya Jaji Makani yanaweza kuwashangaza watu wengi. Zaidi ya yote miaka 46 baada ya Uhuru; wapi tulipo, wapi tunataka kwenda. (Pichani, Amir Jamal, Dereck Brycson, JK Nyerere, Chief Abdallah Fundikira, Gorge Kahama Nyuma: Kushoto Solomon Eliofoo, Rashid Kawawa, Nsilo Swai, Oscar Kambona, Tewa Saidi Tew ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Mkapa na Yona wanyang'anywe Kiwira?

Wakiwa madarakani Rais Benjamini Mkapa na Waziri wake wa Nishati na Madini waliingia ubia na kuanzisha kampuni ya Tanpower Resources. Wakati Yona analiambia Bunge kuwa wanatafuta wawekezaji wa "kufufua" Mgodi wa Makaa ya Mawe wa Kiwira, sirini walikuwa wanapanga yeye na Rais wake kuwa "wawekezaji" hao watakuwa ni wao wawili. Na miezi michache kabla Rais Mkapa hajaachia madaraka, Mgodi wa Kiwira ulikuwa chini ya viongozi hao wawili wakiwa na hisa zaidi ya asilimia 80. Hadi leo hii hakuna ali ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Buriani mzee Kanyama Chiume...

Most of us knew his name by reading his articles and opinions in Mzalendo, Daily News and Uhuru; He was one of the leading nationalists of his time and indeed a patriot of Africa, a true son of our beloved motherland. Mr. Chiume who was born in Malawi and later exiled to Tanzania was a "leader of Nyasaland African Congress and served as the Minister of Education and the Minister for Foreign Affairs in the 1960s." according to one popular website. Beside writing for Tanzania Newspaper he als ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Salamu kwa Siku ya Wanafunzi Duniani - Ukumbi wa DDC

Leo kama mnavyofahamu kulikuwa na makongamano ya wanafunzi jijini Dar-es-Salaam. Moja lilifanyika Ukumbi wa Ubungo Plaza na kuhutubiwa na Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Mhe. Pius Msekwa na lile jingine lililofanyika Ukumbi wa DDC na kuhutubiwa na wasomi mbalimbali na viongozi wa chama cha Demokrasia na Maendeleo akiwemo Mhe. Zitto Kabwe. Nilipata nafasi ya kutuma salamu za mshikamano kwa kongamano la DDC baada ya kuombwa kutuma ujumbe huko. Walioko nyumbani waliupata kwa njia ya maandishi, ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Tuwakatalie watawala wetu?

Wakati umeanza kufika ambapo wananchi waanze kuwakatalia watawala wao!! Nisikilize leo nikifafanua kwanini tuanze kuwakatalia na ni vitu gani hivyo vya kukataa!

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


~ * ~ The Spoken Word - "I Can't Wait" ~ * ~

By. M. M. mwanakijiji Wondering, and hoping, and praying That it’ll all be alright! That my country will rise and be A nation, and it will take its place among the nations Of the World and it’ll be a rightful place. But our rulers keep telling us, just wait! ]They tell us to wait, When we ask about corruption, And when we question their intentions They come back with political intimidation That if we don’t stop, there’ll be a confrontation, So they tell us people! just wait! We hav ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


KLH Exclusive: Mahojiano na Dr. Salim Ahmed Salim

Tarehe 14 Oktoba 2007 ni miaka nane kamili, tangu Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere atutoke na kutuacha wakiwa. Kati ya viongozi na watanzania wachache waliopata kumfahamu Mwalimu kwa karibu na kuwa wasaidizi wake wa karibu ni Dr. Salim A. Salim ambaye aliwahi kushika nafasi mbalimbali za uongozi katika serikali ya Zanzibar na baadaye katika serikali ya Muungano. Baadhi ya nafasi ambazo aliwahi kushika ni pamoja na Ubalozi, Uwaziri (akiwa Waziri Mkuu, Waziri wa Mambo ya Nchi ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Eid Mubarak kwenu Nyote!!!

Napenda kutumia nafasi hii kuwatakia ndugu zetu Waislamu wa Tanzania wanapoungana na Waislamu wengine pote duniani kuadhimisha siku kuu hii ya Eid el Fitr wanapomalizia mfungo Mtukufu wa Ramadhani. Siku ya Jumapili tunatarajia kuwa na matangazo "live" kupitia Bongoradio.com tunapoadhimisha miaka nane tangu Baba wa Taifa atutoke. Hivyo usikose matangazo hayo kuanzia kama saa nane mchana EST sawa na saa tatu za Usiku EAT. Kwa wale Wakristu na watu wa imani nyingine nawakaribisha kwenye ukura ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Nyerere: " Ikulu ni Mzigo, kwanini wanakukimbilia?"

Hii ni sehemu ya pili ya Hotuba ya Mwalimu Mei Mosi 1995. Hapa ndipo alipokuwa mwiba wa serikali ya CCM hasa baada ya kudai kuwa wameacha "Mambo ya Msingi" . Ni katika sehemu hii lile swali muhimu la "kuna biashara gani Ikulu" liliulizwa. NImefanya editing zaidi kidogo ya kupunguza sauti za watu uwanjani ili mwalimu asikike vizuri na ningekuwa na muda zaidi kidogo ningefanya bora zaidi, mniwie radhi kwa mwangwi kidogo.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Nyerere Mei Mosi '95: "Watanzania Mjomba wenu ni nani?"

Ifuatayo ni sehemu ya kwanza ya hotuba aliyoitoa Baba wa Taifa kwenye sherehe za Mei Mosi 1995. Tunapokumbuka miaka nane tangu Mwalimu Nyerere afariki hatuna budi kupitia japo kwa hatua hazina ya hekima yake. Wakati anatoa hotuba hii mwaka 1994 kulikuwa na mgomo wa wafanyakazi, na mwaka 1995 ulikuwa ni mwaka wa uchaguzi na huo ukiwa ni uchaguzi wa kwanza baada ya kurejesha tena mfumo wa vyama vingi. Hivyo, Mwalimu alipokuwa anatoa hotuba hii watu wengi walikuwa wanaonesha nia ya kutaka kw ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Mhe. Moh'd Seif Khatib: "Viongozi hawazomewi, ni uongo!"

Siku ya Jumamosi kwenye matangazo yetu ya moja kwa moja (live) nilipata nafasi ya kuzungumza na Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo wa Serikali ya Tanzania Mhe. Mohammed Seif Khatib (MB). Makubwa tuliyozungumza ni suala zima la tuhuma zilizotolewa na ushirika wa wapinzani tarehe 15 Septemba pale Jijini Dar. Pamoja na hayo tulizungumzia kuhusu suala la Buzwagi na jinsi mwitikio wa wananchi ulivyokuwa na hasa ziara ambazo zimefanywa wiki iliyopita na Mawaziri na Manaibu wao kwenye mikoa ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


CCM ikubali tatizo kwanza...!!

Tangia sakala la "orodha ya ufisadi" lianze, serikali ya CCM imekuwa ikitoa majibu ya kukanganyana na mengine hayaingii akili hata kidogo. Majibu mengine yamejaa kiburi na dharau na mengine inabidi mtu ajiulize "walikuwa wanafikiria nini". Kwa maoni yangu kabla ya viongozi wa serikali na wa CCM kuanza kutoa majibu kuhusu tuhuma kwa viongozi 11, la kwanza ambalo wangelifanya ni kukubali tatizo kwanza, hiki kiburi wanachokionesha kuwa wao hawawezi kukosea na wengine wanadai kuwa wamekuwa w ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Nini kimemsibu Jaji Warioba?

Kama ripoti iliyoandikwa na gazeti la Habari Leo ina ukweli basi kuna kitu kinachoendelea na ambacho bila ya shaka kimemsibu Jaji Warioba kuja na mawazo ya aina hii. Hebu soma na uamue mwenyewe au ni mimi ndiyo nimechanganyikiwa. [b]Mgaya Kingoba HabariLeo; Friday,September 28, 2007 @00:02[/b] WAZIRI Mkuu mstaafu, Jaji Joseph Warioba amesema amekerwa na tabia ya wanasiasa kupakana matope na kuonya kuwa kisingizio cha utawala bora kisitumiwe kutaka kuangusha dola zilizopo madarakani. “Tuk ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


CCM isipuuzie hoja za Wapinzani, wazijibu!

Uongozi wa Chama cha Mapinduzi umeamua kuwa hoja zilizotolewa na watanzania kuhusu masuala mbalimbali hazistahili kujibiwa. Kwa mujibu wa Katibu wa Idara ya Uenezi na Itikadi ya Chama hicho Mhe. Aggrey Mwanri MB (CCM - Siha) CCM haitaenda mahakamani bali itaenda kwa wananchi na kujibu hoja za watanzania hao kwa kuwataka wananchi wazipuuze hoja hizo. Miongoni mwa hoja ambazo Mhe. Mwanri anataka wananchi wazipuuzie ni zile zile za Ubadhirifu wa Benki Kuu, Mikataba ya Madini hususan ule wa Buz ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Rais Mkapa na Matumizi mabaya ya Ikulu - Dr. Slaa

Ifuatayo ni sehemu ya pili ya mahojiano yangu Dr. Slaa kufuatia mkutano wao mkubwa uliofanyika mwishoni mwa wiki. Nimeambatanisha pia orodha na maelezo mliyoyasikia kwenye mahojiano haya ili uweze kupitia moja baada ya nyingine na uweze kutolea maamuzi wewe mwenyewe. Bonyeza Hapa Kudownload

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Kukamatwa wabunge wa CCM, Ishara ya Nyakati?

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa imewatia mbaroni viongozi kadhaa wa Chama cha Mapinduzi kwa tuhuma za kujihusisha na vitendo vya rushwa. Miongoni mwao ni wabunge Michael Laizer wa Longido na Elisa Mollel wa Arumeru Mashariki. Hii ni mara ya kwanza katika miaka ya hivi karibuni kuwa Chama cha Mapinduzi kiko tayari kuwatosha baadhi ya viongozi wake wakubwa. Je inawezekana huu ni mwanzo wa nyakati mpya na ni jaribio la uhuru wa TAKUKURU kufanya kazi zake kwa mujibu wa sheria mpya ya k ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


"CCM wakitaka kuandamana wafanye, tunawangojea!" - Zitto

Ifuatayo basi ni sehemu ya pili na ya mwisho ya mahojiano yangu na Mbunge wa Kigoma Kaskazini Mhe. Zitto Kabwe. Leo anajibu kwa kina alichukuliaje majibu ya Malecela, na kuna mipango gani zaidi ya kuwahamasisha wananchi. Na wapinzani wanaitumia vipi fursa hii ili kujiimarisha? Na ana wito gani kwa wananchi ambao wameanza kuhamasika? Na maswali mengine mengi. Pichani mkutano wa Zitto Jangwani.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


"Mimi ni ishara ya Watanzania kuchoshwa" - Zitto akizunguma na KLH News

Nimepata nafasi ya kuzungumza na Naibu Katibu Mkuu wa Chadema na Mbunge wa Kigoma Kaskazini Mhe. Zitto Zuberi Kabwe. Katika mazungumzo yetu ambayo yamejadili sakata zima la yeye kusimamishwa vikao vya Bunge, Mhe. Zitto pia anazungumzia mwelekeo wa suala hili na mipango ya mbeleni ya kuzidi kuwaamsha Watanzania. Mahojiano yangu naye yamegawanyika sehemu mbili kutokana na urefu wake, na hivyo leo ninarusha sehemu ya kwanza ya mahojiano hayo leo, na sehemu ya pili itakuwa hewani mapema kesho. ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Breaking News! Kikwete azuiwa kuingia Buzwagi!

Wanakijiji wa maeneo yanayozunguka Buzwagi wamezuia msafara wa Rais Kikwete kuingia kwenye eneo ambalo Mgodi wa Buzwagi unatarajiwa kujengwa. Habari zaidi bila ya shaka tutazipata baadaye. Hata hivyo hapa nawaletea sehemu ya Hotuba ya Waziri Mkuu akilihairisha bunge. Bado ninapata matatizo na inaonekana si matatizo ya kompyuta yangu bali ni matatizo ya wao wenyewe podomatic.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


"Kilichofanyika ni kichekesho cha Demokrasia" - Dr. Slaa

Nimepata nafasi ya kuzungumza na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo na Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni Mhe. Dr. Wilbroad Slaa (Karatu) kuhusu kusimamishwa kwa Mhe. Zitto na pia kuhusu yeye kuondoa Bungeni hoja yake binafsi kuhusu Benki Kuu ya Tanzania. Sikupata muda wa kufanyia editing, mixing n.k kutokana na matatizo ya kompyuta za KLH News. Hivyo naweletea jinsi ilivyo, uncut, and unedited.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Kamati Teule yakataliwa - Zitto Apigwa Stop!

Mbunge machachari wa Kigoma Kaskazini Mhe. Zitto Kabwe (Chadema) ambaye aliamua kuleta hoja Bungeni ya kuundwa Kamati Teule ya Bunge ili kuchunguza jinsi Waziri wa Nishati na Madini Mhe. Nazir Karamagi alivyoweza kwenda Uingereza kutia sahini mkataba mpya wa uchimbaji wa madini kabla ya kumalizika upitiaji wa mikataba iliyopo kama ilivyoagizwa na Rais. Hoja hiyo inaonekana imewagawa wabunge kufuatana na itikadi za vyama vyao. Kubwa ambalo inaonekana kuwa limewaudhi baadhi ya wabunge ni ma ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Mabadiliko Bodi ya Mikopo - kutapatapa kwa Msolla?

Wote bila ya shaka mmeshasikia juu ya mswada wa vyombo vya habari, na sitashangaa kuwa mmewahi kusikia sheria mpya ya rushwa. Lakini ni wangapi wamesikia kuhusu mswada wa sheria ya mabadiliko ya Bodi ya Mikopo ya wanafunzi wa Elimu ya Juu? Ni wangapi wanajua kuwa mswada huo ulitangazwa kwenye gazeti la serikali mwezi Juni? Hakuna kitu kibaya kama serikali inayofanya mambo kisiri siri. Hatimaye, tunafahamu kuhusu mswada huo, na leo nachambua mapungufu yake na kunionesha ni jinsi gani kina Ms ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Kaboyonga Ambana Waziri Meghji kuhusu BOT!

Mapema leo Bungeni, Mbunge wa Tabora Mjini Mhe. Siraju Juma Kaboyonga alimbana Waziri wa Fedha Mhe. Zakia Meghji kuhusu gharama za ujenzi wa minara miwili ya benki kuu inayoendelea kujenga ambayo mpaka hivi sasa imegharibu mabilioni ya shiling. Majibu ya Waziri Meghji yamezua maswali mengi zaidi na inaonesha kuwa kuna kitu kinachoendelea. Pia ninawaletea hadithi yangu mpya iitwayo VIVIAN - PETE YA MACHOZI

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Inaudhi serikali inapojifanya mwalimu wa uandishi!

Wakati wa mjadala wa bajeti ya Wizara ya Habari, Michezo na Utamaduni jambo moja lilikuwa dhahiri. Wabunge wengi walijifanya wao ndio walimu wa waandishi wa habari kwa kutoa hoja ambazo bila ya shaka zilionsha upeo wao mdogo wa uhuru, haki, na ,majukumu ya vyombo vya habari. Hata wakati Waziri Mohammed Seif Khatib (Pichani) alipojumuisha hoja za wabunge na kutoa majibu ya maswali yao mbalimbalil alionekana mwenye kuzungumza kana kwamba serikali ndiyo pekee inayojua Uandishi ni fani ya namna ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Hoja za Uraia wa nchi mbili tuzikubali?

Kwa muda mrefu sasa mjadala wa uraia umekuwa ukiendelea nchini. Hoja hizo ambazo zinalengo la kubadili sheria ya Uraia nchini zimepata mtetezi mkubwa Bungeni ambaye ni Mbunge wa Singida Kaskazini Mhe. Lazalo Samuel Nyalandu (Pichani)ambaye kutokana na kuishi kwake nje ya nchi kwa muda mrefu ameweza kuwakakilisha mawazo ya watanzania wengi walioko ugenini ambao wanataka Tanzania ibadili sheria yake ya Uraia. Hata hivyo, je hoja zinazotolewa ni nzito kiasi cha kuweza kufanya Tanzania iruhusu ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Tanzania inahitaji Katiba Mpya au Mabadiliko tu ya Sheria?

Mjadala umefunguliwa, ili kujenga jamii yenye haki zaidi na usawa zaidi mbele ya sheria na kuwa na mfumo wenye usawa zaidi katika siasa za nchi yetu je, Tanzania tunahitaji Katiba Mpya au tufanye tu mabadiliko kwa kuzingatia mapendekezo ya Tume ya Jaji Nyalali na tume ya Jaji Kisanga.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


CCM iliahidi kutatua suala la Kadhi - Itaweza?

Jana Bungeni suala la mahakama ya kadhi mkuu wa Tanzania liliibuliwa tena katika jitihada za wapinzani kuitaka serikali ya CCM kutimiza ahadi yake ya kulitafutia ufumbuzi suala hilo kwa maislahi ya waislamu wa Tanzania. Je hoja zinazotolewa zinaridhisha? Je majibu yanayotolewa na serikali ya CCM yanatosheleza? Je kwa kuzingiatia mazingira ya Tanzania bara na katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania mahakama ya kadhi yaweza kuundwa bila kuleta mgongano wa kisheria au kimahusiano ya kidini? ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Hatima ya waliokanwa Ukraine kujulikana leo?

Tafadhali tembelea tovuti hii kutwa nzima wakati tunafuatilia hotuba ya Waziri wa Sayansi, Teknolojia na Elimu ya Juu Mhe. Prof. Peter Msolla. Nina uhakika kuwa suala la vijana hawa kama halitakuwemo kwenye bajeti basi litakuwemo wakati wa majadililiano ya Bunge kama Kamati ambapo wabunge hupitia bajeti vifungu kwa vifungu. NI matumaini yangu kuwa leo jambo hilo litafikia mwisho wake kwa Bunge kuingilia kati na kuwaingiza vijana hawa kwenye bajeti ya mwaka huu na kuwafanya waendelee na maso ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Upotevu wa Mabilioni Benki Kuu, Mrema alisema kweli?

Madai ya upotevu wa mabilioni ya fedha toka Benki Kuu hayakuanza leo. Kwa wale wanaokumbuka watakumbuka kuwa madai ya upotevu wa mabilioni ya fedha ilikuwa ni mojawapo ya mambo ambayo yalimuengua Bw. Augustino Mrema toka serikali CCM na baadaye kujikuta akiwa upinzani Miezi michache kabla ya kuibuka tena kwa tuhuma za kupotea mabilioni ya fedha nilizungumza na Bw. Mrema kuhusu mambo mbalimbai yaliyokuwa yakimhusu yeye kisiasa na kiuongozi. Haya ni mahojiano yangu naye ambapo anatumia muda m ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Tuwaachie Nchi watawala wetu?

Tangu mtiririko wa kashfa uanze kuiandama serikali ya Tanzania hakuna hatua hata moja ya uhakika iliyochukuliwa kukabiliana na tuhuma hizo na hakuna mtu yeyote ambaye amewajibishw kwa kulisababisha Taifa hasara zisizo za lazima. Kuanzia kashfa kubwa ya Loliondo, IPTL, Ndege ya Rais, Tanesco, TTCL, KIA, Tanesco, Dawasa, Madini, Richmond, BOT na sasa Helikopta za kijeshi, serikali yetu imetia pamba masikioni kiasi cha kwamba haitaki kuambiwa wala kusikia. Hoja zinazotolewa Bungeni na wapinzan ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Mhe. Anne Kilango na wanamapinduzi wasiobadilika!

Juzi Mbunge wa Same Mhe. Anne Kilango Malecela (Pichani) alizungumza Bungeni na kwa kutumia kauli kali alisema kuhusu jinsi serikali ilivyolegeza taratibu za ukaguzi wa makontena "Mimi nasema `No`, tutaimaliza nchi sasa". Jambo moja ambalo amelisahau ni kuwa CCM imeachana na mawazo ya kimapinduzi zamani na hawako tayari kujua kuwa tunaishi katika kipindi cha mabadiliko makubwa ya kizazi. Na ninyi mnaosikiliza matangazo haya mnaishi katika wakati muhimu na ambao si wa kujutia bali wa kutupa ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Twawapa Notisi watawala wetu! - Tanzania waliyoizoea...

Bunge hili halitakuwa kama mabunge mengine yaliyotangulia na huko tunakokwenda kutakuwa na mambo mengi zaidi ya kulifanya Bunge hili lichangamke na kuwajibika. Ni kwa sababu hiyo basi kitendo cha Dr. Slaa kuwasomea taarifa ya tuhuma ya umafia wa baadhi ya viongozi wetu ni kitendo ambacho kimewashtua watawala wetu na mshtuko huo ulijionesha kwa sura zao. Walipigwa na butwaa na mshangao kama watu waliojikuta wakinyeshewa na mvua na hapakuwa na pakukimbilia isipokuwa chini ya mwembe. Wakiwa ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Dr. Slaa Azua Bungeni suala la Mafia wa Tanzania!

Jana Bungeni, Mbunge wa Karatu Mhe. Wilbroad Slaa amezungumzia kuhusu ripoti ambayo imekuwa ikisambazwa kwenye mtandao kuhusu kundi la wahalifu wakimataifa ambao wamejikita katika utawala wa serikali na wameshirika vilivyo katika mikataba mbalimbali na masuala mbalimbali ambayo yameisababisha serikali yetu "kupoteza" mabilioni ya shilingi. Kama ripoti hiyo ina ukweli au la ni uamuzi wa msomaji mwenyewe. Vinginevyo, inawezekana kuwa amefungua kisanduku cha Pandora ambacho hawezi tena kukifun ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Umepata matumaini?

Waziri wa Fedha Mhe. Zakia Meghji (pichani) amewasilisha bungeni bajeti ya serikali ya mwaka 2007/2008. Bajeti hii ni ya makadirio ya mapato na matumizi ya serikali kwa mwaka huu mpya wa fedha. Wakati bajeti ya mwaka jana ilikuwa kali kwa wananchi na kwa vile ilikuwa ni bajeti ya kwanza ya utawala wa Rais Kikwete basi makosa ya hapa na pale na mapungufu ya hapa na pale yalitarajiwa. Mwaka mmoja baadaye matarajio ya watu yako juu zaidi kuwa Bajeti hii itakuwa ni ya kumpa nafuu mwananchi wa k ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Dr. Noordin Jella "Serikali iunde tume Huru"

Kati ya watu wote waliokwisha zungumzia suala hili la vijana Ukraine hakuna mwenye mtazamo wenye kutupa mwanga zaidi kama Dr. Noordin Jella. Yafuatayo ni mahojiano yangu naye na katika mahojiano hayo anapendekeza Rais aunde tume huru itakayochunguza ukweli wa jambo hili na kuhakikisha kuwa kama vijana hawa kweli walipewa mikopo na ilitakiwa iwafuate huko Ukraine wao wakitangulia, basi haki yao wapewe. Kama kuna makosa yalifanyika kati ya Dr. Jella au Wizara, vijana hawa wasiadhibiwe kwa "v ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Wabunge na Bunge "Lao"..

Bunge la Jamhuri linaanza kikao chake cha bajeti hivi karibuni. Kuna mambo kadhaa ambayo yanaendelea yanayolihusisha Bunge hili ambayo kwa kweli yanatufanya tujiulize kama kweli Bunge letu lina ubavu wa kuisimamia serikali au wajibu wake ni kujiongezea posho na marupurupu tu. - Kujiongezea posho ya mafuta ya shilingi milioni 480 kwa mwezi wa wabunge ni halali kweli? - Kufungia vyombo vya habari kwenye mikutano ya Kamati za Bunge, wanataka kuficha nini? nyongeza ya posho? - Kuacha serikali ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Exclusive: Mabinti Ukraine nao Wazungumza!

Tumeshawasikia kina kaka wakielezea hali yao huko Ukraine baada ya kutekelezwa na serikali. Je dada zao nao waliotelekezwa huko wanasemaje? Licha ya serikali kuwakana vijana hawa wote bado wanahitaji msaada wetu, msaada wa mtu yeyote mwenye mapenzi mema na anayewataki mema vijana hawa. Tafadhali ili kupata maelezo jinsi ya kuwasaidia: Bonyeza Hapa

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Ridhiwani achukua fomu.. CCM inatengenezeana njia?

Je kitendo cha watoto wa viongozi wa CCM kama kama kina Nape Nnauye, Zainab Kawawa, Vita Kawawa, Adam Malima, Hussein Mwinyi n.k kuanza kushika nafasi za uongozi katika CCM na kile cha kina Ridhiwani na wenzake kutaka kuingia kwenye nafasi hizo ni jambo ambalo watanzania waliangalie kwa hofu kwani CCM wameanza kurithishana vyeo au tuwaache vijana hawa watelekeze haki yao ya kikatiba na tusiwahukumu kwa makosa au matendo ya wazazi wao? Pichani Ridhiwani Kikwete akichukua fomu huku Bagamoyo, ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Prof. Mwandosya awakatalia wawekezaji Ngorongoro!

Kati ya vitu ambavyo hutokea mara chache Tanzania ni kitendo cha Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Profesa Mwandosha kumkatalia mwekezaji kujenga hoteli kwenye ukingo wa Crater ya Ngorongoro licha ya mamlaka nyingine husika kukubali mpango huo. Alichofanya Prof. Mwandosya kimenifanya nijiulize swali, hivi "kila anachotaka mwekezaji ni lazima apewe"? Je, kitendo hiki cha Mwandosha ni mfano wa mtu kujali nchi au ndio mazingaombwe yale yale?

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Mwenge wa Uhuru - Tuukimbize au tuukimbie?

Tangu kusimikwa juu ya mlima Kilimanjaro usiku ule wa kuamkia Uhuru, Watanzania tumeendelea kukimbiza mwenge huu kutukumbusha tunu hii iliyobora zaidi kwa mwanadamu, tunu iliyomfanya mtu mmoja kusema "nipe Uhuru au nipe Kifo". Hata hivyo kwa kadiri miaka inavyokwenda hatuna budi kujiuliza kama kweli ipo haja ya kukimbizana na moto huu au umefika wakati tuanze kuukimbia!! Pichani mwenge wa Uhuru ukiwa wilayani Karagwe, Kagera mwaka 2003

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Tuhuma dhidi Rais Mkapa: Ajibu asijibu?

Tangu kuondoka kwake madarakani Rais Mstaafu Ndg. Benjamin William Mkapa amekuwa akikabiliwa na tuhuma mbalimbali kuhusu utajiri alionao na hasa kuhusu baadhi ya matukio yaliyotokea wakati wa utawala wake. Hata hivyo, yeye mwenyewe hayuko tayari kujibu tuhuma hizo au hata kuonesha kuwa amezisikia na anazifanyia kazi. Swali ambalo bila ya shaka linawagawa Watanzania ni kama Rais Mkapa akae chini na kujibu tuhuma hizo au aendelee kuzipuuzia kuwa ni kelele za watu wenye wivu.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Watanzania mnaitwa, mtaitika? Serikali imekurupuka kujibu!

Serikali imetoa tamko lake na inaendelea kushikilia uzi ule ule wa kutowatambua vijana wetu waliokwama Ukraine. Hata hivyo, wakati umefika wa kuwasaidia vijana hawa kupitia akaunti iliyofunguliwa ili waendelee kusoma na si kurudishwa nyumbani wakiwa wameshindwa. Nimejibu hoja za serikali zilizotolewa jumatatu ambazo kwa kile zimeonesha hawakufuatilia suala hili kabisa na wamekurupuka tu kujibu kwa kusoma habari magazetini! Ili kuchangia hawa vijana tafadhali fuata maelekezo kama yanavyopat ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Flaviana, Ukraine, na Viongozi wetu!

Leo sitaki kusema mengi, kwani maneno mengi wakati mwingine huchosha. Hakikisha unampigia kura binti yetu Flaviana Matata. Why? pick any reason!

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Kikwete: "Kama (wizara) wangeshindwa wangeniambia!"

Hatimaye jana jumatano, ubalozi wa Uingereza kule Kiev, Ukraine umepata majibu toka Ubalozi wa Uingereza Tanzania ambao walikuwa wanafuatilia suala hili la vijana 29 waliokatishwa masomo yao baada ya serikali kushindwa kutimiza ahadi ya kuwasomesha. Jibu lililopatikana toka Wizara ya Sayansi, Teknolojia na Elimu ya juu ni kuwa serikali haiwatambui vijana hao, haihusiki kuwarudisha nyumbani na lolote litakalowapata ni shauri yao. Baada ya kuhakikisha jibu hilo na Ubalozi huo, nilijikuta sina ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Wanafunzi kujisalimisha Ubalozi wa Uingereza, Ukraine!

Wanafunzi wa kitanzania wapatao 29 waliotelekezwa na serikali ya Rais Jakaya Kikwete kwenye vyuo vya nchini Ukraine hatimaye wameamua kufanya kile walichotishia miezi michache iliyopita, nacho ni kujisalimisha na kuomba hifadhi kwenye Ubalozi wa Uingereza jijini Kiev, nchini Ukraine. Ubalozi huo tayari umeshakubali kuwapokea vijana hao mapema asubuhi. Uamuzi huo umefikiwa baada ya serikali ya Tanzania chini ya Wizara ya Sayansi na Elimu ya juu kuwakana wanafunzi hao na kutowatambua licha ya ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Halmashauri ya Taifa ya CCM ina uwezo huu?

Wiki iliyopita iliripotiwa na vyombo vya habari kuwa Chama cha Mapinduzi kupitia Halmashauri yake Kuu ya Taifa kitaanza kuwaita na kuwahoji watendaji wa serikali ili kuona kama wanatekeleza vyema Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2005-2010. Kwa nje nje jambo hilo halina tatizo lakini tukiliangalia kwa karibu tutaona kuwa kama litaachwa kusimama basi Tanzania tunaanza kurudi nyuma kwenye mtindo wa Chama Kimoja cha siasa na ni hatari kwa mgawanyo wa madaraka ulioanishwa vyema kikatiba. Pichan ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Msolla ajiuzulu

Leo namuondolea uvivu Prof. Msolla. Soma makala yangu kwenye Tanzania Daima.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Nakulilia Nchi Yangu!

Siwezi kusema mengi kuhusu hili, sikiliza wewe mwenyewe!!

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Wazazi wa wanafunzi Ukraine Wazungumza! Sehemu I

Nimezungumza na baadhi ya wazazi wa wanafunzi ambao leo hii bado wanapiga kambi kwenye ya ofisi za Ubalozi wa Uingereza Ukraine. Wanafunzi hao wamegoma kuondoka hapo hadi serikali iseme na kutatua tatizo lao. Wazazi nao mioyo yao imevunjika na wana ujumbe wa wazi kwa Rais Kikwete. Binafsi nimetoa mchango wangu kidogo wa kuwasaidia kwa chakula na matumizi hawa wanafunzi 20 hadi suala hili litatuliwe. Wakati tunasubiri serikali itatue (siyo kushughulikia) tatizo hili natoa wito tena muungane ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


TAKURU na Mkataba wa Richmond: Alichokwepa Hosea!

Wiki moja iliyopita, Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia Rushwa (TAKURU) Bw. Edward Hosea alitoa maamuzi kuhusu mkataba wa Richmond ambao serikali ya Rais Kikwete iliungia mwaka jana katika jitihada za kutafuta ahueni ya tatizo la nishati lililoikabili nchi yetu. Mkataba huu ulipoingiwa maswali mengi yaliulizwa na shutuma nyingi zilitolewa na mojawapo ya shutuma hizo ni kuwa kuna rushwa ilitumika. Bw. Hosea katika maelezo yake kwa vyombo vya habari alihitimisha mjadala huo kwa kusema kuwa "kati ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Wazazi wa wanafunzi wanazungumza Sehemu II

Ni maendelezo ya mazungumzo na wazazi wa vijana hawa.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Vita vya Mawaridi - Una mbavu? shikilia...

Leo nawapa burudani ya kituko kimoja toka katika moja ya radio za hapa US. Natumaini itawapa weekend nzuri.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Dr. Hussein Mwinyi: "Muungano wetu ni wa Watu!"

Muungano wetu hatimaye umetimiza miaka 43. Licha ya misuko suko ya hapa na pale na migogoro ambayo ingeweza kabisa kutishia kuuvunja muungano huu, hata hivyo bado muungano unadumu na unaendelea kuwa nuru ya ndoto za waasisi wa Bara la Afrika la kuwa siku moja bara letu lingeweza kuungana. Muungano wetu ni muungano ambapo licha ya majaribio ya watu mbalimbali kujaribu kuudhofisha umeendelea kuwa imara na thabiti. Hata hivyo, kwa kadiri siku zinavyokwenda ndivyo tunavyoona jamii yetu na watu ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Bunge linapotukanwa tena!

Yafuatayo ni marudio ya matangazo niliyoyafanya mwaka jana baada ya Bunge kuambiwa kuwa haliwezi kupitia mikataba. Jambo hili limerudiwa tena na kwa vile mada ni ile ile basi badala ya mimi kurudia tena kuzungumzia hapa nimeona nirudie hili nililolisema wakati ule. Hata hivyo kuhusu hili la sasa nimeandika makala ambayo mtasoma siku ya Jumatano kuhusu suala hili. Picha ya ofisi ndogo ya Bunge, Zanzibar.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


"Mungu Usiwabariki viongozi wetu"!

Katika wimbo wa Taifa tunaimba na kuomba Mungu "wabariki viongozi wetu" itakuwaje kama tukianza kumuomba Mungu asiwabariki viongozi hao? Leo ninatoa sala na dua mbele ya Mwenyezi Mungu aache kuwabariki viongozi wetu, kwani kila walipobarikiwa, wamegeuza baraka hizo laana kwa nchi yetu!!

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Utawala wa Kikwete na Taifa la waliokata tamaa!?

Watanzania lazima tuangalie sana. Sasa hivi katika nchi yetu kuna hatari ya mamilioni ya watu kukata tamaa na kupoteza matumaini. Endapo tutafikia mahali (au kama tayari tumeshafikia) ambapo wananchi wa nchi hii watakata tamaa ya uongozi wao na kuamua "kila mtu na lwake" basi tujue kabisa hatima ya nchi yetu iko matatani. Picha ya watoto wa shule ya msingi, je hawa wakikata tamaa, Taifa lina hatima gani? Je Rais Kikwete anaweza kuturudishia matumaini kwa kizazi cha sasa na kijacho?

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Twamkumbuka Edward Sokoine - Mtu wa watu

Leo ni miaka 23 tangu Waziri Mkuu Edward Moringe Sokoine atutoke ghafla na kuacha simanzi na wingu la huzuni. Siku ile ya machozi na majonzi imebakia katika kumbukumbu za Watanzania wengi kama vile jana. Mfano wake ni kumbukumbu ya Wamarekani waliposikia habari za kuuawa kwa Rais John F. Kennedy. Kila mtu aliyekuwa mtu mzima wakati ule anakumbuka vizuri siku hiyo alikuwa wapi na alikuwa anafanya nini. Je pengo aliloliacha marehemu limeanza kuzibwa? Je kuna kiongozi yoyote ambaye anakaribi ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Sitaki Spika ajifanye yeye Papa au Ayatollah!

Kitendo cha Spika kutumia uwezo wake kunyamazisha mjadala Bungeni ni kitendo ambacho lazima kionekane kwa mwanga unaostahili, yaani ni kitendo cha kimabavu, matumizi mabaya ya madaraka, na kinachopakana na tabia za kiimla. Inawezekanaje mtu mmoja kuamini kuwa ana uwezo wa kuwanyamazisha wawakilishi wa watu kuzungumzia jambo fulani kwa vile tu jambo hilo linamhusu yeye? Inakuwaje mlalamikiwa ndio akawa mkata shauri!!? Walisema ukistaajabu ya Musa, utaona ya Farao! (Pichani Mhe. E. Lowassa - ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Tanzania ni yetu sote!

Kuna baadhi ya watu ambao kwa namna fulani wanafikiri kuwa au wamejiambia hadi wakaamini kuwa Tanzania ni ya kwao peke yao na uzao wao! Hili halikubaliki, tutalipinga, na kukumbushana kuwa nchi hii ni yetu sisi sote na wakati umefika kwa wale waliomadarakani kuanza kuufanyia kazi ukweli huu! Picha ya nembo ya Taifa, tunaweza kuona katika pande mbili za ngao wamesimama mwanamme upande wa kushoto na mwanamke upande wa kulia wakiwa sawa! Hata hivyo katika nembo haisemwi hao wanawakilisha watu ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Polisi wetu wameshindwa?

Baada ya matatizo ya kiufundi hatimaye tumefanikiwa kuweka matangazo mapya. Hata hivyo watu wa podomatic wamenisumbua sana kiasi cha kufikia kuhamisha podcast hii kwenda mahali pa uhakika. Tutawajulisha pindi mambo ya kikamilika.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Homa ya Bonde la Ufa: Serikali imechukua hatua zinazostahili?

Leo nina mambo kama matano hivi ya kuzungumza ambayo ningezungumza wiki iliyopita. Kubwa kati ya hayo ni tatizo la Homa ya Bonde la Ufa ambayo inazidi kuenea taratibu nchini. Serikali imechukua hatua kadhaa lakini najiuliza kama hatua hizo zinatosha au la. Pichani, ni ramani ya mgawanyo wa Homa ya Bonde la Ufa, rangi ya Bluu ni nchi ambazo zimewahi kuwa na mlipuko mkubwa wa Ugonjwa huu, na Kijani ni nchi ambapo kumeripotiwa kuwepo kwa ugonjwa huu ingawa si kwa kiasi kikubwa. Tusipoangalia ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Tuzungumzie Taifa Stars

Kufungwa na Senegal ndio mwisho wa soka au tuwe na matumaini

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Hoja za mahabusu zisitufikishe pabaya!

Hili suala la mahabusu kugoma kushuka kutoka kwenye makarandinga wakidai kuwa na wao kesi zao ziharakishwe kama ya Ditopile siyo suala la kupuuzia, kudharau au kuwaachia polisi tu walishughulikie. Mwisho wa suala hili inawezekana kuwa ni mwisho mbaya. Ni matarajio yangu kuwa serikali ya Kikwete haitasitasita kulipatia suala hili ufumbuzi unaostahili.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Kesi ya Ditopile - DPP aanza Mazingaombwe!!

Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) ameamua kubadili mashtaka yanayomkabili Bw. Ditopile Mzuzuri anayetuhumiwa kumuua kijana Hassan Mbonde kwa kumlipua na risasi akiwa ndani ya daradara alilokuwa akiendesha. Mashtaka ya sasa ni yale ya "kuua bila kukusudia". Mwendesha mashtaka ameda kuwa Watanzania hawaelewi sheria ila yeye peke yake!! Mimi sikubaliani naye na ninazijibu hoja alizozitoa hadharani kuhusu kwanini mashtaka sasa ni yale ya "kutokukusudia". Sizungumzii hatia ya mtuhumiwa kwani hiyo ni ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Happy Valentine - Kwa wale wapendwao!

Leo basi nawaletea burudani a vibao sita vya mahaba na mapenzi katika kusherehekea siku kuu ya Valentine. Kwanini, tunasherehekea unaweza kuniuliza, I have no idea!!! labda kuna mtu anadhani tunahitaji kukumbushwa kupenda...! Anyway, kwa wale mpendao na mpendwao, heri ya Valentine!!

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Haki Elimu Imeikosea Nini Serikali?

Shirika la HakiElimu lilipigwa marufuku kufanya utafiti na kutangaza mambo yoyote yahusuyo shule za Tanzania. Agizo hilo limerudiwa tena hivi karibuni kwa baraka za Ofisi ya Waziri Mkuu. (pichani, mojawapo ya mabango ya Haki Elimu)

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Miaka 30! CCM Hongera! Lakini....

Tarehe 5/2/2007 itakuwa imetimia miaka thelathini tangu Chama cha Mapinduzi kuzaliwa baada ya vyama vya TANU na ASP kuvunjwa. Sherehe kubwa zimezinduliwa na Rais wa Zanzibarna zitahitimishwa na Rais Kikwete siku ya Jumapili (siku yenyewe inaangukia Jumatatu) Bila ya shaka tutasikia maneno matamu na ya kuvutia na watu mbalimbali watatuma pongezi kwa chama hicho. Na mimi basi kwa namna yangu nimeonelea nitume pongezi zangu kwa chama hicho.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Sheria ya Rushwa Tumfurahishe Nani? Wafadhili...???

Bunge la Jamhuri ya Muungano linatarajiwa kujadili muswada wa sheria dhidi ya rushwa. Hata hivyo, inavyoonekana sheria hii kupitishwa kwake ni kwa ajili ya kuwafurahisha wafadhili wachache ambao wametishia kutotupa misaada hadi sheria hii ipitishwe. Kama sheria hii haitungwi kwa ajili ya kujenga matumaini ya Watanzania, basi sheria hii itashindwa kama zilivyoshindwa sheria nyingine. Hata hivyo, hii haipaswi kuwa hivyo. Je Rais Kikwete ataliongoza Taifaletu kushinda tatizo hili la rush ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Mahojiano na Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa

Yafuatayo ni mahojiano na Dr. Asha-Rose Mtengeti Migiro Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa. Kabla ya kuteuliwa kushika wadhifa huo wa pili kwa madaraka katika UM, Dr. Migiro alikuwa ni Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Tanzania.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


phone post

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


phone post

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Magufuli: Shujaa au Mjanja kama wengine?

Suala la uuzwaji wa nyumba za serikali kwa vigogo mbalimbali lilizua maswali toka mwanzo na hivi sasa tunaona kuwa maswali yale yalikuwa na msingi. Hata hivyo mmoja wa "Askari wa Miamvuli" wa serikali ya Mkapa leo anatuhumiwa kukiuka taratibu za kazi na kujipendelea katika mtiririko mzima wa ununuaji nyumba za serikali. Je huu ni mtihani mwingine kwa Kikwete, na nini kifanyike kuepusha manung'uniko yasiyo ya lazima. Pichani, baadhi ya nyumba za serikali ambazo nyingine kama hizo zimeuzwa b ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Mahojiano na Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo wa TZ

Baada ya kufanya mazungumzo na mtengenezaji wa filamu ya "Darwin's Nightmare" leo ninawaletea mahojiano ya kina na Waziri wa Habari, Michezo na Utamaduni wa Tanzania Mhe. Mohammed Seif Khatib (MB) - pichani. Kwenye picha kubwa na picha ya kisanii ya Uwanja mpya wa Taifa unaoendelea kujengwa. Nilimuuliza Mhe. Khatib habari za filamu hiyo, timu ya Taifa na Uwanja wa Taifa.

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


An Interview with Director H. Sauper of "Darwin's Nightmare"

"Send a message to Tanzanians I'm not your enemy and (Tanzania) is the country that I like it very much!" Declares Director Hubert Sauper whose film "Darwin's Nightmare" has caused so much uproar in Tanzania since President Kikwete condemned it two weeks ago. Director Sauper spoke to the host of KLH News (http://mwanakijiji.podomatic.com) Mr. M. M. Mwanakijiji on Friday following the news that the Parliament of Tanzania has also issued a resolution condemning the movie. In this candid and ...

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website


Kupitia upya mikataba haitoshi!

Serikali imetanga kuundwa kwa chombo ambacho kitapitia mikataba yote ya madini ambayo serikali iliyopita iliingia. Lengo ni kuhakikisha kuwa mikataba hiyo ina vipengele vyenye kunufaisha pande zote zinazohusika na utekelezaji wa mikataba hiyo. Hata hivyo kupitia mikataba peke yake haitoshi! Ni lazima twende zaidi ya kupitia vipengele vya mikataba....

Listen | Listen in your iPhone | Download | View full cache | Visit Website