Search for PodcastsRegister | Sign In
Podcast
Internet Radio

Podcast Directory:
Browse Podcasts
Add your Podcast
Remove a Podcast
Search for Podcasts
Podcast Directory
by Country
by Language
by Buzz
by Popularity
by Category
by Tags
by Region
by City
on a Google Map



Podcast Help:
What is Podcasting
Creating an XML
Podcast Hosting
Podcast Software
Firefox Plugin
Podcast Hardware




About Us:
Podcast Advertising
Contact Us
Copyright Issues
Help Wanted



Running and Fitness

Run Saturday


Internet Radio:
Find
State
Country
Language
Music
Sports
Regions
Popularity

Trumix.com
Our New Site
Internet Radio
Podcasts
Create a Playlist



Discount Gold Offer

Nani ashinde, nani ataamua mshindi? Episode | Sauti ya Mwanakijiji

PodcastDirectory / News and Politics / News
PodcastDirectory / Regions / AF / Tanzania



Sauti ya Mwanakijiji

Primary Format :
News

Also Listed as:

User Tags:

User Votes:

RSS Feed
Website

Visit Methings.com for the most recent listings of:

Nani ashinde, nani ataamua mshindi?


Nani ashinde, nani ataamua mshindi?

Play Now -->

DATE : Thu, 07 May 2009 04:42:19 GMT
Entered in Database : 2009-05-07 04:42:19
length : 12968228
Link to the Show / Show Notes

itunes pic

Ni mgongano wa kihistoria ambao ulipaswa kutokea. Ni mgongano ambao hutokea mahali popote panapokuwa na tofauti kubwa kati ya watawala na watawaliwa. Ndivyo ilivyokuwa kwenye Mapinduzi ya Ufaransa, Mapinduzi ya Marekani na Mapinduzi ya Bolshevik (Urusi).

Ni yale yale yaliyotokea na kusababisha mapinduzi ya Cuba yaliyomuingiza Castro madarakani. Ndiyo! Ni yale yale yaliyotokea pia kwenye mapinduzi ya Zanzibar!

Migongano ya namna hiyo asili yake mara zote ni pale wananchi wanapotambua kuwa hawana usawa na watawala wao na ya kuwa tofauti ya maisha yao na yale ya watawala ni kubwa mno na ya kwamba mwananchi wa kawaida anajikuta hana nafasi yoyote aidha ya kufanikiwa au ya kuweza kuishi maisha yenye utu, usawa, haki na heshima.

Nchi chache zimeweza kupitia mgongano huo kwa njia ya nguvu (kama mifano niliyotoa) au kama ilivyotokea huko Ukraine na Georgia miaka ya karibuni kwa njia ya nguvu ya umma.

Tanzania yetu inapitia mgongano huo katika hatua zake za awali. Silaha ambayo wananchi wanatumia leo hii ni nguvu yao ya hoja na wanatarajiwa kubadilisha serikali yao kwa nguvu ya kura.

Hata hivyo hilo halitakuwa rahisi kwani dalili yote inaonesha kuwa watawala hawako laini kuruhusu mabadiliko makubwa ya kiutawala yenye kupendelea wananchi wa kawaida. Hivyo, mgongano unaendelea. Swali ni nani ashinde? Na ni nani ataamua mshindi!?

Nisikilize:


Play in your Iphone